“Kama wewe ni Mwana wa Mungu, ujitupe chini; kwa maana imeandikwa: ‘Mungu atawaamuru wamalaika wake na watakubeba katika mikono yao, kusudi muguu wako usijikwae juu ya jiwe.’ ”
Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”
Alipokwisha kukaa Antiokia kwa siku chache, akaondoka kule, akapita muji kwa muji toka katika inchi ya Galatia mpaka katika inchi ya Furigia, na kule akawatia wanafunzi nguvu.
Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.
Kwa hiyo ilimupasa afanane na wandugu zake katika mambo yote, kusudi apate kuwa Kuhani Mukubwa anayekuwa mwenye huruma na mwaminifu katika kazi yake mbele ya Mungu, na kwa njia hiyo zambi za watu zisamehewe.