Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 22:42 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

42 “Baba, kama ukitaka, ninakuomba uniondolee mbali kikombe cha mateso. Lakini isikuwe mapenzi yangu ndiyo yafanyike, lakini yako.” [

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 22:42
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu nikasema: “Ninakuja. Katika kitabu imeandikwa juu yangu.


Amuka, ewe Yerusalema! Amuka usimame wima! Yawe amekukunywesha kikombe cha kasirani yake, nawe umekikunywa mpaka tone la mwisho, mpaka ukayumbayumba.


Bwana, Yawe, Mungu wako, anayewatetea watu wake, anasema hivi: Nimekuondolea kikombe cha kuyumbisha, hautakunywa tena kikombe cha kasirani yangu.


Yawe, Mungu wa Israeli, akaniambia hivi: Twaa toka katika mukono wangu kikombe hiki cha divai kinachojaa kasirani yangu uyakunyweshe mataifa yote ninayokutuma kwao.


Katika siku zile Yesu akasema: “Ee Baba, Mwenyeji wa mbingu na dunia, ninakushukuru kwa maana mambo uliyoyaficha kwa watu wenye hekima na elimu, umeyafunua kwa wanaokuwa wadogo.


Ndiyo, Baba, hayo yote ni kutokana na mapenzi yako.


Yesu akawaambia: “Hamujui kitu munachoomba. Munaweza kubeba muzigo wa mateso nitakaoubeba?” Nao wakamujibu: “Tunaweza.”


Kisha akajitenga mbali kidogo nao, akainama uso chini. Akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama ikiwezekana, ninakuomba uniondolee mbali kikombe hiki cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”


Akawaacha tena kwa mara ya pili, akaomba akisema: “Ee Baba yangu, kama kikombe hiki cha mateso hakiwezi kupita mbali nami, bila mimi kukikunywa, basi mapenzi yako yafanyike!”


Yesu akawaacha tena, na kwenda kuomba kwa mara ya tatu, akirudilia maombi yale yale.


Ufalme wako ukuje; mapenzi yako yafanyike katika dunia kama inavyokuwa mbinguni.


Akasema: “Ee baba! Yote yanawezekana kwako; ninakuomba uniondolee mbali hiki kikombe cha mateso. Lakini isikuwe kama vile mimi ninavyotaka, lakini kama vile wewe unavyotaka.”


Halafu Yesu akasema: “Baba uwasamehe, kwa maana hawajui jambo wanalofanya.” Waaskari wakagawanya nguo zake kwa kuzipigia kura.


Lakini Yesu akamwambia Petro: “Rudisha upanga wako katika kifuko chake! Inanipasa kunywa kikombe cha mateso Baba yangu alichonitayarishia.”


Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma na kutimiza kazi yake.


“Siwezi kufanya kitu kwa mafikiri yangu mwenyewe. Ninahukumu tu kama vile Mungu anavyoniambia na hukumu yangu ni ya haki, kwa sababu sitafuti kufanya mapenzi yangu, lakini mapenzi ya yule aliyenituma.


Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.


Tulipoona kwamba amekataa shauri letu, tukanyamaza na kusema: “Mapenzi ya Bwana yafanyike.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ