Naye akawaambia: “Lakini sasa, yule anayekuwa na feza azitwae, na anayekuwa na mufuko autwae vilevile. Na yeyote asiyekuwa na upanga, auzishe nguo yake apate kuununua.
Yesu akajibu: “Ufalme wangu si wa dunia hii. Ufalme wangu ungekuwa wa dunia hii, watumishi wangu wangenipigania kusudi nisitolewe kwa Wayuda. Lakini sasa ufalme wangu si wa hapa katika dunia.”
Lakini sisi ni watu wa muchana, tunapaswa kuwa wakadirifu. Tunapaswa kushikamana na imani na upendo kama vile nguo ya chuma ya kukingia kifua, nalo tumaini letu la wokovu kama vile kofia ya kutulinda.