Luka 22:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
26 Lakini isikuwe hivi katikati yenu. Lakini yule anayekuwa mukubwa kati yenu sherti akuwe mudogo zaidi, na yule anayekuwa mwongozi sherti akuwe kama mutumishi.
Basi Yesu akaikaa, akawaita wanafunzi wake kumi na wawili na kuwaambia: “Mutu anayetaka kuwa wa kwanza anapaswa kujiweka wa mwisho kuliko wote na kuwa mutumishi wa wote.”
na kuwaambia: “Anayemupokea mutoto mudogo kama huyu kwa jina langu, ananipokea mimi. Naye anayenipokea mimi, anamupokea yule aliyenituma. Kwa maana yule anayekuwa mudogo kati yenu ndiye anayekuwa mukubwa.”
Musifuate mwenendo wa siku hizi, lakini muache Mungu awabadilishe kwa kugeuza upya nia zenu, hata mukuwe na mawazo mapya. Kwa hiyo mutaweza kutambua mapenzi ya Mungu. Mutajua mambo gani yanayokuwa mema, yanayomupendeza Mungu na yanayokuwa makamilifu.
Na hivi vilevile, ninyi vijana, munapaswa kuwatii hao wazee. Ninyi wote munapaswa kuwa na unyenyekevu, mupate kutumikiana; maana Maandiko Matakatifu yanasema: “Mungu anawapinga wenye kiburi, lakini anawajalia wanyenyekevu neema.”