Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 22:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kisha Yesu akatwaa kikombe, akakibariki na kusema: “Mutwae kikombe hiki na mukigawanye kati yenu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 22:17
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitamutolea sadaka ya divai kwa kumushukuru maana ameniokoa. Nitaomba kwa jina la Yawe.


Umenitayarishia karamu mbele ya waadui zangu. Umekipakaa kichwa changu mafuta. Kikombe changu umekijaza tele.


Hakuna atakayechangia chakula na yule aliyekufiwa kwa kumufariji, wala kumupatia kinywaji cha kumufariji kwa ajili ya kukufiwa na mama au baba yake.


Kisha kuwaamuru watu waikae juu ya majani, Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Akamega ile mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakaigawanya kwa kundi la watu.


Kisha akatwaa ile mikate saba na zile samaki, akamushukuru Mungu, akaimega na kuwapa wanafunzi wake wavigawanye kwa watu.


Walipokuwa wakikula, Yesu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema: “Mutwae na mukule, huu ni mwili wangu.”


Walipokuwa wakikula, akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema: “Mutwae, huu ni mwili wangu.”


Halafu akatwaa mukate, akaubariki, kisha akaumega na kuwapa akisema: “Huu ni mwili wangu [unaotolewa kwa ajili yenu. Mufanye hivi kwa kunikumbuka.”


Kisha Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Halafu akaimega, akawapa wanafunzi waigawanyie watu.


Mutu yeyote anayeshugulika juu ya siku fulani, anafanya hivi kwa kumutukuza Bwana. Yule anayekula kila chakula, anafanya vile kwa kumutukuza Bwana; maana anamushukuru Mungu kwa ajili ya chakula chake. Na asiyekula kila chakula anafanya hivi vilevile kwa kumutukuza Bwana na kumushukuru Mungu.


tunapokunywa kikombe ambacho kwa ajili yake tunamutolea Mungu shukrani, basi kwa njia ya kikombe kile hatuungani na damu ya Kristo? Nasi tunapomega mukate na kuukula, kwa njia hiyo, mukate ule hautuungi na mwili wa Kristo?


Kwa maana haya ndiyo mafundisho niliyopokea kutoka kwa Bwana, nami niliyotoa kwenu: katika usiku ule Bwana Yesu alipotolewa, alitwaa mukate,


Mutakula na kushiba, mutamushukuru Yawe, Mungu wenu, kwa inchi nzuri aliyowapa.


Mara moja mutakapoingia katika muji, mutamukuta mbele hajakwenda kwenye nafasi ya ibada kwenye mulima kwa kula. Maana watu hawatakula mpaka kwanza yeye abariki sadaka. Kisha wale walioalikwa watakula. Hivyo muende haraka; mutakutana naye sasa hivi.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ