Kisha kuwaamuru watu waikae juu ya majani, Yesu akatwaa ile mikate mitano na samaki mbili, akainua macho mbinguni, akamushukuru Mungu. Akamega ile mikate, akawapa wanafunzi wake, nao wakaigawanya kwa kundi la watu.
Mutu yeyote anayeshugulika juu ya siku fulani, anafanya hivi kwa kumutukuza Bwana. Yule anayekula kila chakula, anafanya vile kwa kumutukuza Bwana; maana anamushukuru Mungu kwa ajili ya chakula chake. Na asiyekula kila chakula anafanya hivi vilevile kwa kumutukuza Bwana na kumushukuru Mungu.
tunapokunywa kikombe ambacho kwa ajili yake tunamutolea Mungu shukrani, basi kwa njia ya kikombe kile hatuungani na damu ya Kristo? Nasi tunapomega mukate na kuukula, kwa njia hiyo, mukate ule hautuungi na mwili wa Kristo?
Mara moja mutakapoingia katika muji, mutamukuta mbele hajakwenda kwenye nafasi ya ibada kwenye mulima kwa kula. Maana watu hawatakula mpaka kwanza yeye abariki sadaka. Kisha wale walioalikwa watakula. Hivyo muende haraka; mutakutana naye sasa hivi.”