Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 21:37 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

37 Yesu alikuwa akipitisha muchana katika hekalu akihubiri, na usiku alikuwa akienda kulala kwenye mulima wa Mizeituni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 21:37
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Siku hiyo, atasimama kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa upande wa mashariki wa Yerusalema. Mulima ule utagawanywa kwa sehemu mbili na bonde pana litatokea toka upande wa mashariki mpaka wa magaribi. Nusu moja itaelekea upande wa kaskazini na nusu ingine kusini.


Yesu na wanafunzi wake wakakaribia kufika Yerusalema upande wa kijiji cha Betefage, karibu na mulima wa Mizeituni. Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake,


Kisha akawaacha, akatoka inje ya muji wa Yerusalema, naye akaenda Betania na kulala kule.


Nao walipokwisha kuimba, wakaondoka kwenda kwa mulima wa Mizeituni.


Kisha Yesu akawaambia watu wale: “Mumekuja na panga na magongo kwa kunikamata kama watu wanavyokwenda kumukamata munyanganyi? Siku zote niliikaa ndani ya hekalu, nikifundisha, nanyi hamukunikamata.


Kesho yake, walipotoka Betania, Yesu akasikia njaa.


Ilipokuwa magaribi, Yesu na wanafunzi wake wakatoka katika muji ule.


Siku zote nilikuwa pamoja nanyi, nami nilifundisha ndani ya hekalu, nanyi hamukunikamata. Lakini mambo haya yamefanyika kusudi Maandiko Matakatifu yatimizwe.”


Alipokaribia kufika katika kijiji cha Betefage na cha Betania upande wa mulima wa Mizeituni, Yesu akawatuma wawili kati ya wanafunzi wake, akiwaambia:


Alipokaribia Yerusalema kwenye mutelemuko wa mulima wa Mizeituni, kundi zima la wanafunzi wakafurahi na kuanza kumusifu Mungu kwa sauti kubwa kwa ajili ya miujiza yote waliyoiona.


Yesu alikuwa akifundisha kila siku ndani ya hekalu. Lakini wakubwa wa makuhani na walimu wa Sheria pamoja na wakubwa wa watu wakatafuta kumwua.


Yesu akatoka na kwenda kwa mulima wa Mizeituni kama ilivyokuwa desturi yake. Na wanafunzi wake wakamufuata.


Siku sita mbele ya Pasaka, Yesu alifika Betania, kwao Lazaro, yule mutu Yesu aliyemufufua.


Yuda, yule aliyekuwa amemutoa, alijua pahali pale, kwa sababu Yesu alikuwa akikutana kule mara nyingi pamoja na wanafunzi wake.


Kisha mitume wakarudi Yerusalema tokea kwenye mulima wa Mizeituni unaokuwa karibu na muji huo kwenye umbali wa yapata kilometre moja.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ