Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 21:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 “Mujilinde vizuri, kusudi musilemewe na kutafuta kula ulafi, kulewa na kusumbukia maisha. Kama si vile, Siku ile ya kurudia kwa Kristo itawafikia kwa rafla

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 21:34
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, tumuleweshe baba kwa divai, kusudi tupate kulala naye na kudumisha uzao kwa kupata watoto kwa njia yake.”


Basi, usiku ule vilevile wakamulewesha baba yao kwa divai, kisha yule binti mudogo akakwenda akalala naye. Lakini baba yake hakujua wakati binti yake alipolala naye, wala wakati alipoondoka.


Basi, Yakobo akakwenda kutwaa wana-mbuzi wawili na kuwaletea kwa mama yake. Naye akatayarisha chakula kitamu sawa vile baba yake Isaka alivyopenda.


Maangamizi yawapate wao kwa rafla, wanaswe katika mutego wao wenyewe, watumbukie katika shimo lao wenyewe!


Macho ya kiburi na moyo wa majivuno vinaonyesha wazi zambi ya waovu.


Usikuwe mumoja kati ya walevi wa divai, wala walafi wenye kupenda nyama,


Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.


Lakini kuna wengine waliolewa divai na kuyumbayumba kwa sababu ya pombe kali; makuhani na manabii wamelewa pombe kali, wamevurugika kwa divai. Wanayumbayumba kwa pombe kali; maono yao yamepotoka, wanajikwaa katika kutoa hukumu.


Uasherati, divai mupya na ya zamani vinaondoa maarifa.


Munapoingia ndani ya hema la mukutano, wewe na wana wako musikunywe divai wala kileo chochote, kama sivyo mutakufa. Hili litakuwa sharti ambalo vizazi vyenu vyote wanapaswa kulifuata siku zote.


Pahali zile mbegu zilipoanguka katika miiba, ni mufano wa wale wanaosikia Neno la Mungu, lakini masumbuko ya dunia hii na udanganyifu wa mali vinasonga lile neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.


“Mujiangalie vizuri ninyi wenyewe, kwa maana watawapeleka mbele ya tribinali kwa kuwahukumu na kuwapiga fimbo katika nyumba za kuabudia. Vilevile mutapelekwa mbele ya wakubwa na wafalme kwa ajili yangu, kusudi mutoe ushuhuda wangu mbele yao.


lakini masumbuko ya dunia hii, udanganyifu wa mali, na tamaa za namna nyingine vikiwaingia, vinasonga lile Neno linalokuwa ndani yao na kulizuiza kuzaa matunda.


Bwana akamujibu: “Marta! Marta! Kwa nini unahangaika na kusumbuka kwa ajili ya vitu vingi?


Kwa hiyo ninyi vilevile mukuwe tayari, kwa sababu Mwana wa Mutu atarudia saa musiyozania.”


Kwa sababu hii mujiangalie vizuri. “Kama ndugu yako akikosa, umwonye, na akigeuka toka katika zambi zake, umusamehe.


sawa mutego. Kwa maana Siku ile itawafikia watu wote wa dunia.


Yesu akawajibu: “Muangalie vizuri, musidanganywe. Watu wengi watakuja wakijiita kwa jina langu, wakisema kwamba wao ndio Kristo, nao wakati umetimia. Ingawa vile, musiwafuate.


Na mbegu zilizoanguka katika miiba ni mufano wa wale wanaosikia, lakini masumbuko, utajiri na raha ya dunia vinawasonga hata wanashindwa kutoa matunda yanayokomaa.


Lakini niliwaandikia kwamba musishirikiane na mutu anayejiita ndugu mwamini, akiwa mwasherati, mwenye tamaa, mwenye kuabudu sanamu, mutukanaji, mulevi au munyanganyi. Na zaidi ya ile musichangie chakula na mutu wa namna hii.


wizi, wenye tamaa, walevi, watukanaji, wanyanganyi, watu wale wote hawatapata urizi katika Ufalme wa Mungu.


kutambikia sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, kasirani, mapingano, matengano, ubaguzi,


Yawe hatasamehe mutu huyo, nayo hasira ya Yawe na wivu wake vitamuwakia mutu huyo. Laana zote zilizoandikwa katika kitabu hiki zitamupata, naye Yawe atafuta kabisa jina la mutu huyo kutoka katika dunia.


Musijisumbue juu ya neno lolote, lakini katika kila neno mutoe mahitaji yenu kwa Mungu, mukimwomba, mukimusihi na kumushukuru.


Muangalie vizuri, kusudi hata mutu mumoja asijikoseshe mwenyewe kupata neema ya Mungu, wala asikuwe sawa shina la mumea unaotoa matunda machungu na kuleta fujo kati yenu na kuambukiza watu wengi.


Siku Bwana atakaporudi, itatimia kama vile mwizi anavyokuja. Siku ile mbingu zitatoweka kwa shindo kubwa, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitayeyuka. Dunia na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake vitateketezwa.


Kwa sababu hiyo, wapendwa wangu, mukiwa munangojea mambo yale, mufanye bidii apate kuwakuta safi bila kosa lolote na mukae na amani pamoja naye.


Basi ukumbuke mafundisho uliyopokea na yale uliyosikia. Uyashike na kugeuka toka zambi zako. Kama usipokesha, nitakuja kama mwizi, wala hautajua saa nitakapokuja kwako.


Abigaili aliporudi kwake, alimukuta Nabali akifanya karamu kubwa katika nyumba yake kama ya kifalme. Nabali alikuwa akifurahi sana ndani ya moyo maana alikuwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia neno lolote mpaka asubui.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ