Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 21:25 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

25 “Vitambulisho vitaonekana katika jua, mwezi na nyota. Na hapa katika dunia mataifa yatakuwa na uchungu, na kushikwa na wasiwasi kwa ajili ya mungurumo na musukosuko wa bahari.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 21:25
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo hatutaogopa kitu chochote, hata dunia ikiyeyuka na milima kutikisika kutoka bahari,


Nyota na vikundi vyake katika anga hazitaangaza; jua linapochomoza litakuwa giza, na mwezi hautatoa mwangaza wake.


Aha! Ngurumo ya watu wengi! Wananguruma kama bahari. Aha! Mulio wa watu wa mataifa! Yanatoa mulio kama wa maji mengi.


Kisha mwezi utafezeheka, nalo jua litapata haya ya kuangaza, maana Yawe wa majeshi atatawala kule Yerusalema katika mulima Sayuni; ataonyesha wazee wa watu wake utukufu wake.


Siku hiyo, watanguruma juu ya Israeli kama uvumi wa bahari iliyochafuka. Atakayeiangalia inchi kavu ataona giza tupu na taabu, mwangaza utafunikwa na mawingu.


Mimi ni Yawe, Mungu wako, ninayechafua bahari, zoruba yake ikinguruma; Yawe wa majeshi, ndilo jina langu!


Niliangalia dunia, nikaona imekuwa ukiwa na tupu; niliangalia mbingu, nazo hazikukuwa na mwangaza.


Wakati huo, Mikaeli, malaika mukubwa, anayekuwa mulinzi wa watu wako, atatokea. Halafu kutakuwa wakati wa taabu sana kuliko nyakati zingine zote tangu mataifa yalipoanza kuwa katika dunia. Lakini, wakati huo, kila mumoja wa watu wako ambaye jina lake limeandikwa katika kitabu cha uzima, ataokolewa.


Mutu muzuri zaidi kati yao ni kama michongoma, naye mwenye usawa zaidi ni hatari kama upango wa miiba. Siku iliyongojewa ya azabu yao imefika. Na sasa mahangaiko yamewapata.


“Mara moja kisha mateso ya siku zile, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza, nyota zitaanguka toka mbinguni na vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.


Tangia saa sita ya muchana, giza lilikuwa katika inchi yote mpaka saa tisa.


“Lakini katika siku zile kisha mateso yale, jua litatiwa giza, mwezi hautaangaza,


Na halafu wakati ule Mwana wa Mutu ataonekana akikuja katikati ya mawingu kwa uwezo mwingi na kwa utukufu.


Ilipokuwa saa sita ya muchana, giza likakuwa katika inchi yote mpaka saa tisa.


Wamoja watauawa kwa vita na watapelekwa kuwa wafungwa katika inchi za mataifa yote. Vilevile mataifa mengine yatautawala Yerusalema mpaka nyakati zao za kuutawala zitakapokwisha.”


Watu watazimia kwa ajili ya hofu, wakingojea mambo yatakayotokea katika dunia, kwa maana vyote vyenye nguvu katika mbingu vitatikiswa.


Nami nitafanya maajabu juu katika mbingu na vitambulisho chini katika dunia: kutakuwa damu, moto na moshi mwingi.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ