Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 21:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 Lakini muendelee kuvumilia, maana kwa njia ile mutaokoa uzima wenu.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 21:19
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tulia mbele ya Yawe, umungojee kwa uvumilivu; usihangaike juu ya wale wanaofanikiwa, ndio watu wanaojaliwa katika mipango yao mibaya.


Nikasikia hayo, matumbotumbo yangu yakatetemeka. Midomo yangu inatetemeka kwa hofu, mifupa yangu inateguka, miguu yangu inatetemeka. Ninangojea kwa utulivu siku ile ya hasara, ambayo inawafikia wale wanaotushambulia.


Na watu wote watawachukia kwa ajili yangu. Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ataokolewa.


Lakini atakayevumilia mpaka mwisho ataokolewa.


Nao udongo muzuri walimopanda mbegu, ni mufano wa watu wanaosikia neno la Mungu na kulishika kwa moyo mwema na kwa uhaki. Ndio wale wanaovumulia hata wanatoa matunda mazuri.


Na yote yaliyoandikwa zamani katika Maandiko Matakatifu yameandikwa kwa ajili ya kutufundisha sisi, kusudi tuendelee kuchunga tumaini kwa njia ya kuvumilia na kufarijiwa sawa tunavyofundishwa katika Maandiko Matakatifu.


Wale wanaofanya matendo mema bila kuchoka na kutafuta toka kwa Mungu utukufu, heshima na uzima usiokuwa na mwisho, Mungu atawapa uzima wa milele.


Zaidi ya hii, tunafurahi vilevile kwa ajili ya mateso tunayopata, kwa sababu tunajua kwamba mateso yanaleta uvumilivu,


na uvumilivu unaleta uaminifu kamili na uaminifu ule unaleta tumaini.


Lakini tukitumainia kitu tusichokiona, tunakingojea kwa uvumilivu.


Kwa maana tunakumbuka mbele ya Mungu Baba yetu namna munavyotumika kwa imani na munavyojisumbua na kazi kwa ajili ya upendo wenu. Vilevile tunakumbuka namna tumaini lenu katika Yesu Kristo linavyokuwa imara.


Bwana aongoze mafikiri yenu katika upendo wa Mungu na katika uvumilivu tunaopewa na Kristo.


Munapaswa kuvumilia, kusudi mutimize mapenzi ya Mungu, na kuweza hivi kupewa kile mulichoahidiwa.


Lakini tunatamani sana kwamba kila mumoja kati yenu aendelee kuonyesha bidii ile mpaka mwisho, kusudi mambo yale munayotumainia yapate kutimizwa.


Hivi kisha kungojea kwa uvumilivu, Abrahamu akapokea yale Mungu aliyomwahidi.


kwa maana munajua kwamba kupimwa kwa imani yenu kunawaletea uvumilivu.


Lakini sherti uvumilivu ule utimize kazi yake, kusudi mupate kuwa wakamilifu na watimilifu wasiopungukiwa na kitu.


ukadirifu juu ya elimu yenu, uvumilivu juu ya ukadirifu, kushikamana na ibada juu ya uvumilivu,


Mimi ni ndugu yenu Yoane. Kwa njia ya kuungana na Yesu, ninashirikiana nanyi katika mateso, katika ufalme wake na katika kuvumilia. Mimi nilikuwa nimepelekwa katika kisanga kinachoitwa Patimo, kwa sababu nilihubiri Neno la Mungu na ukweli ulioshuhudiwa na Yesu.


Mutu yule aliyekusudiwa kuwa mufungwa, atafungwa; na yule aliyekusudiwa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanapaswa kuwa wavumilivu na wenye imani.”


Kwa sababu hiyo, watu wa Mungu wanaoshika amri za Mungu na kumwamini Yesu wanapaswa kuwa wavumilivu.


Kufuatana na vile ulivyojichunga katika uvumilivu sawa nilivyokuagiza, mimi vilevile nitakuchunga na hasara wakati itakapokuja katika dunia yote kwa kuwajaribu wakaaji wake.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ