Tena kama vile Yawe alivyosema, Nebukadneza alitwaa mali yote iliyokuwa ndani ya nyumba ya Yawe, na ndani ya nyumba ya kifalme. Akakatakata vyombo vyote vya zahabu ambavyo Solomono mufalme wa Israeli alitengeneza. Vyombo hivyo vilikuwa ndani ya hekalu la Yawe.
Nikachagua watu hawa kuwa walinzi wa gala: kuhani Selemia, Zadoki mwandishi na Pedaya, Mulawi. Hanani mwana wa Zakuri mujukuu wa Matania akakuwa musaidizi wao. Walikuwa waaminifu na kazi yao ilikuwa kuwagawanyia wandugu zao mahitaji yao.
Wakubwa wa makuhani wakaokota zile feza na kusema: “Kufuatana na Sheria yetu hairuhusiwi kuweka feza kama hizi ndani ya sanduku ya hekalu kwa sababu feza hizi ni za damu.”
Yesu alisema maneno haya wakati alipokuwa akifundisha katika hekalu, kwenye sanduku za kuwekea matoleo. Hakuna mutu aliyemufunga, kwa sababu wakati wake ulikuwa haujatimia.
Kisha, wakauchoma kwa moto muji wa Yeriko na kila kitu kilichokuwa mule isipokuwa feza, zahabu, vyombo vya shaba na vya chuma; hivyo viliwekwa katika hazina ya nyumba ya Yawe.