Kila mutu anayesema vibaya juu ya Mwana wa Mutu atasamehewa, lakini kila mutu anayesema vibaya juu ya Roho Mutakatifu, hatasamehewa katika ulimwengu huu, wala katika ule unaokuja.
Basi bwana wa yule mulinzi akamusifu kwa sababu alitenda kwa werevu. Kwa maana watu wa dunia hii wanatengeneza maneno yao na wenzao kwa werevu sana kuliko watu wanaopenda kuishi katika mwangaza.”
Siku zile watu walikuwa wakikula na kunywa, wakioa na kuolewa mpaka ilipotimia siku ile Noa alipoingia ndani ya chombo. Halafu mvua kubwa ikanyesha na kuwaangamiza wote.
Ni sawasawa inavyosemwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu hii, mume ataacha baba yake na mama yake na kuungana na muke wake, nao wawili watakuwa mwili mumoja.”