Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 20:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Basi wakaanza kumuvizia Yesu, wakatuma wapelelezi waliojifanya kuwa kama watu wazuri kusudi wamunase katika masemi. Na kwa njia ile waweze kumutoa katika mikono ya watawala wa inchi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 20:20
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo alituma watu kule Tekoa kusudi wamutafutie mwanamuke mwenye hekima. Walipomuleta, akamwambia: “Ujifanye sawa vile mwenye kuwa na kilio. Vaa nguo za kilio, usijipakae mafuta, lakini ujifanye kama mwanamuke ambaye amekuwa katika kilio kwa muda murefu.


Warafiki na wenzangu wanaepuka kuona mateso yangu, na wandugu zangu wanakaa mbali nami.


Mumwambie Mungu: “Matendo yako ni ya ajabu! Kwa nguvu yako kubwa waadui zako wanaishiwa nguvu.


Ningewashinda waadui zao haraka; ningenyoosha mukono juu ya wapinzani wao.


Nami nilikuwa kama kondoo mupole anayepelekwa kuchinjwa; sikujua kwamba shauri walilofanya lilikuwa juu yangu. Wao walisema: Tuuharibu muti pamoja na matunda yake, tumwue apate kusahaulika katika dunia, jina lake lisikumbukwe tena.


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


Ninasikia watu wengi wakinisingizia uongo, nao wananipanga jina la Kitisho Kila Pahali! Wengine wanasema: Tumushitaki, Tumushitaki! Rafiki zangu wapenzi wote wanangojea kwa hamu nianguke! Wanasema: Labda atadanganyika, tupate kumunasa na kumulipiza kisasi.


Danieli akaonekana kuwa bora kuliko wale wasimamizi wengine na wakubwa wote kwa maana alikuwa na roho njema. Hivyo mufalme akakusudia kumupa uongozi wa ufalme wote.


Wakamufunga, wakamupeleka na kwenda kumutoa kwa liwali Pilato.


Watu waliokuwa mule wakamuchunguza Yesu kusudi waone kama atamuponyesha mutu yule kwa siku ya Sabato, wapate sababu ya kumushitaki.


wakimupima kusudi wapate kumunasa katika masemi yake.


Wale wapelelezi wakamwuliza: “Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha maneno ya kweli. Vilevile wewe hauangalii cheo cha mutu, lakini unafundisha juu ya namna ya kuishi ambayo Mungu anaamuru kufuata.


Basi watu wale hawakuweza kumunasa katika neno lolote mbele ya watu, lakini wakashangaa na jibu lake, nao wakanyamaza.


Na kwa sababu ya tamaa yao mbaya ya mali, walimu hawa wa uongo watajipatia faida juu yenu kwa njia ya maneno ya uongo. Lakini tangia zamani hukumu yao imekwisha kutangazwa, nao hawatakawia kuangamizwa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ