Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 20:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Atakuja na kuwaua wale walimaji. Na kisha atawapatia walimaji wengine shamba lile.” Watu waliposikia maneno hayo, wakasema: “Isitufikie vile hata kidogo.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 20:16
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati siku za mavuno zilipotimia, akawatuma watumishi wake kwa wale walimaji kusudi wamupatie sehemu yake ya mavuno.


Nao wakamujibu: “Atawaua hao watu wabaya pasipo huruma, naye atapatana na walimaji wengine kwa kutunza shamba lake na kumupatia sehemu yake ya matunda kwa wakati wa mavuno.”


Halafu mufalme akakasirika. Akawatuma waaskari wake kuwaua wale wauaji na kuteketeza muji wao kwa moto.


Kisha Yesu akauliza: “Basi yule mwenye shamba la mizabibu atafanya nini? Yeye atakuja na kuwaua wale walimaji. Na kisha atawapatia walimaji wengine shamba lile.


Na sasa kwa ngambo ya wale waadui zangu walionikataa mimi kuwa mufalme wao, muwalete hapa na kuwaua mbele yangu.’ ”


Halafu wakamukamata wakamwua na kutupa maiti yake inje ya shamba.” Kisha Yesu akauliza: “Basi yule mwenye shamba atawatendea walimaji wale namna gani?


Halafu Paulo na Barnaba wakawaambia bila woga: “Ilitupasa kwanza kuhubiri Neno la Mungu kwenu. Lakini kwa kuona mumelikataa na kujihesabu ninyi wenyewe kwamba uzima wa milele haufai kwenu, basi tunashugulika na watu wa mataifa mengine.


Basi ninauliza: Mungu amewatupilia watu wake? Hapana hata kidogo! Maana kwa ngambo yangu, mimi ni Mwisraeli wa uzao wa Abrahamu, toka kabila la Benjamina.


Basi ninauliza: Waisraeli wamejikwaa hata wakaanguka kabisa? Hapana hata kidogo! Lakini kutokana na kosa la Waisraeli, watu wa mataifa mengine wamepata kuokolewa, kusudi wayasikilie wivu.


Basi ni kusema kwa sababu ya imani ile tunaitupilia Sheria? Hapana hata kidogo! Lakini tunasimamisha Sheria.


Hapana hata kidogo! Sherti Mungu ajulikane kuwa mwenye ukweli, na kila mutu kuwa mwongo, kama inavyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Ee Mungu, sherti ujulikane kuwa mwenye haki katika masemi yako. Nawe ushinde wakati unaposhitakiwa.”


Hapana hata kidogo! Ingekuwa vile, namna gani basi Mungu angeweza kuhukumu dunia?


Ni nini basi? Tufanye zambi kwa sababu sisi hatuishi chini ya Sheria, lakini chini ya uwongozi wa neema ya Mungu? Hapana hata kidogo!


Hapana hata kidogo! Sisi tuliokufa kwa ajili ya zambi, namna gani tutaweza tena kuishi katika zambi?


Basi ni kusema kile kinachokuwa kizuri kimeniletea kifo? Hapana hata kidogo! Ni zambi ndiyo iliyoniletea kifo. Lakini kusudi zambi ionekane kuwa zambi kweli kweli, ilipitia kwa njia ya kile kinachokuwa kizuri kwa kusababisha kifo changu. Hivi kwa njia ya amri ile, zambi ilizidi kujikamilisha kuwa zambi kabisa.


Tuseme nini basi? Sheria ni zambi? Hapana hata kidogo! Lakini pasipo Sheria singejua zambi ni nini. Kwa maana singejua kutamani ni nini kama Sheria isingesema: “Usitamani.”


Basi tuseme nini? Mungu hafuati haki? Hapana hata kidogo!


Munajua kwamba miili yenu ni viungo vya mwili wa Kristo. Basi nitatwaa kiungo cha mwili wa Kristo kwa kukifanya kuwa kiungo cha kahaba? Hapana hata kidogo!


Sasa tunapotafuta kuhesabiwa haki katika kuungana na Kristo, inaonekana kwamba sisi nasi ni wenye zambi sawa watu wa mataifa mengine. Jambo hili linaonyesha ya kama Kristo anatumika kwa ajili ya kuendelesha zambi? Hapana hata kidogo!


Basi, ni kusema kwamba Sheria haipatani na ahadi za Mungu? Hapana, hata kidogo! Kama kungetolewa Sheria yenye uwezo wa kuleta uzima kwa watu, basi mutu angehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya Sheria.


Na mimi kwa ngambo yangu sitaki kujivuna, isipokuwa tu kwa ajili ya musalaba wa Bwana wetu Yesu Kristo. Maana kwa njia ya musalaba huo, ninahesabu dunia kama vile imekwisha kufa na mbele ya dunia mimi ninahesabiwa kama vile mufu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ