Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 2:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Na kwa rafla malaika wa Bwana akawatokea, na mwangaza wa utukufu wa Bwana ukawazunguka. Nao wakaogopa sana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 2:9
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nao makuhani walishindwa kutumika ndani kwa sababu ya wingu hilo; kwa sababu utukufu wa Yawe uliijaza nyumba ya Yawe.


Wakati Haruni alipokuwa akizungumuza na Waisraeli wote pamoja, watu wote wakaangalia kule katika jangwa na mara moja utukufu wa Yawe ukaonekana katika mawingu.


Tena, kesho asubui mutaona utukufu wa Yawe maana ameyasikia manunguniko muliyomunungunikia. Sisi ni nani hata mutunungunikie?”


Litachanua maua kwa wingi kama waridi, litashangilia na kuimba kwa furaha. Mungu atalijalia utukufu wa milima ya Lebanoni, uzuri wa mulima Karmeli na wa bonde la Saroni. Watu watauona utukufu wa Yawe, watauona ukubwa wa Mungu wetu.


Kisha utukufu wa Yawe utafunuliwa, na watu wote pamoja watauona. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Simama, ee Sayuni uangaze; maana mwangaza unatokea kwa ajili yako, utukufu wa Yawe unakuangazia.


Basi, nikasimama na kwenda katika bonde. Nikiwa huko nikauona utukufu wa Yawe ukiwa umesimama huko kama utukufu ule niliokuwa nimeuona karibu na muto Kebari; nami nikaanguka uso mpaka chini.


Naye alipokuwa angali akifikiri juu ya maneno hayo, malaika wa Bwana akamutokea katika ndoto na kumwambia hivi: “Wewe Yosefu, mwana wa Daudi, usiogope kumwoa muchumba wako Maria, kwa maana mimba yake imetokana na uwezo wa Roho Mutakatifu.


Malaika akamufikia kwenye nyumba yao na kumwambia: “Salamu kwako, wewe uliyejaliwa neema kutoka kwa Mungu! Bwana yuko pamoja nawe.”


Na katika pande zile, kulikuwa wachungaji kule katika mbuga wakichunga kondoo zao usiku.


Walipokuwa wakifazaika kwa ajili ya jambo hili, mara moja watu wawili waliovaa nguo zenye kungaa wakawatokea.


Isaya alisema maneno haya kwa sababu aliona kwa mbali utukufu wa Yesu, naye alisema habari zake.


Kwa rafla malaika wa Bwana akatokea na mwangaza ukajaa ndani ya chumba kile. Malaika akamutikisa Petro na kumwamusha, akimwambia: “Simama upesi!” Nayo minyororo ikaanguka toka kwenye mikono yake.


Kwa maana usiku malaika wa Mungu, ninayekuwa mutu wake na ninayemwabudu, alinitokea


Lakini usiku malaika wa Bwana akafungua milango ya kifungo, akawaondosha mitume mule na kuwaambia:


Sisi wote ambao uso haukufunikwa, tunaonyesha kama kioo utukufu wa Bwana. Kwa hiyo, tunabadilishwa kwa kufanana na Bwana, nasi tunapita toka utukufu mumoja hata utukufu mwingine unaokuwa mukubwa zaidi tena. Kwa maana kazi hii inatimizwa na Bwana ndiye Roho.


Yule Mungu aliyesema: “Mwangaza uangaze katika giza,” ndiye aliyeangaza ndani ya mioyo yetu, na kutuwezesha kufahamu utukufu wa Mungu unaongaa kwenye uso wa Kristo.


Hakika siri ya ibada yetu ni kubwa: Yeye alitokea kwa mufano wa mutu, alishuhudiwa na Roho Mutakatifu kuwa mwenye haki. Alionekana na wamalaika. Alitangazwa katikati ya mataifa. Aliaminiwa popote katika dunia. Na alinyanyuliwa mbinguni katika utukufu.


Na mambo yale yaliyoonekana yalikuwa ya kuogopesha sana, hata Musa akasema: “Ninaogopa na kutetemeka!”


Kisha mambo hayo, nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni. Yeye alikuwa na uwezo mukubwa; na dunia yote ilingaa kwa utukufu wake.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ