5 Alienda kujiandikisha kule pamoja na muchumba wake Maria ambaye alikuwa mimba.
Katika siku zile, Augusto, mufalme wa Roma akatoa amri kwamba wafanye hesabu ya watu wa utawala wake wote.
Watu wote walienda kujiandikisha, kila mumoja katika muji wake wa kuzaliwa.
Basi Yosefu naye vilevile akaondoka katika muji Nazareti, wa jimbo la Galilaya, na kwenda Yudea katika muji wa kuzaliwa wa mufalme Daudi, unaoitwa Betelehemu. Alienda kule kwa sababu alikuwa mutu wa ukoo wa Daudi.
Walipokuwa kule Betelehemu, wakati wake wa kuzaa ukatimia.