Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 2:49 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

49 Yesu akawajibu: “Kwa nini mulinitafuta? Hamujui kwamba ninapaswa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 2:49
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu nikasema: “Ninakuja. Katika kitabu imeandikwa juu yangu.


Yawe wa majeshi anasema: Ninamutuma mujumbe wangu anitangulie kunitengenezea njia. Bwana munayemutafuta atalifikia hekalu lake kwa rafla. Mujumbe munayemutazamia kwa hamu kubwa atakuja na kutangaza agano langu.


Yesu akaingia ndani ya hekalu, naye akawafukuza watu wote waliokuwa wakiuzishia na kununulia vitu vyao ndani yake. Akapindua meza za wale waliobadilisha feza na viti vya wachuuzi wa njiwa.


Wazazi wake walipomwona, wakashangaa sana. Mama yake akamwuliza: “Mutoto wangu, kwa nini umetufanyia kama hivi? Mimi na baba yako tulikutafuta tukiwa na wasiwasi.”


Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma na kutimiza kazi yake.


Lakini Yesu akawajibu: “Baba yangu anatumika wakati wote, nami ninatumika vilevile.”


Lakini mimi nina ushuhuda mukubwa zaidi kuliko ule uliotolewa na Yoane. Maana sasa mambo ninayofanya ndiyo Baba aliyoniamuru kutimiza, nayo yananishuhudia na kuonyesha kwamba yeye amenituma.


Kwa sababu nimeshuka toka mbinguni kusudi nifanye mapenzi ya yule aliyenituma, wala si mapenzi yangu.


Yule aliyenituma ni pamoja nami; hakuniacha peke yangu, kwa sababu siku zote ninafanya maneno yanayomupendeza.”


Imetupasa kufanya kazi za yule aliyenituma wakati kungali muchana, kwa sababu usiku unakaribia, wakati mutu asipoweza kutumika.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ