Luka 2:39 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
39 Wakati wazazi wa Yesu walipokwisha kutimiza kanuni zote zilizoagizwa na Sheria ya Bwana, wakarudia pamoja naye Galilaya, katika muji wao wa Nazareti.
Lakini Yesu akamujibu: “Ukubali kufanya hivi sasa. Kwa maana ni kwa njia hii tutatimiza mambo yote yanayokuwa ya haki mbele ya Mungu.” Basi Yoane akakubali.
Basi Yosefu naye vilevile akaondoka katika muji Nazareti, wa jimbo la Galilaya, na kwenda Yudea katika muji wa kuzaliwa wa mufalme Daudi, unaoitwa Betelehemu. Alienda kule kwa sababu alikuwa mutu wa ukoo wa Daudi.
Yesu akafika Nazareti, nafasi alipokomalia. Siku ya Sabato ilipotimia akaingia katika nyumba ya kuabudia kama ilivyokuwa desturi yake. Akasimama kwa kusoma Maandiko Matakatifu;
Yesu akawaambia: “Hakika mutaniambia fumbo hili: ‘Muganga, ujiponyeshe wewe mwenyewe!’ Na vilevile mutaniambia hivi: ‘Tumesikia mambo yote uliyotenda katika muji Kapernaumu, basi uyafanye hapa vilevile katika muji wako.’ ”