Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 2:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 alikuwa amemufunulia kwamba hatakufa mbele hajamwona Kristo wa Bwana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 2:26
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wafalme wa dunia wanajitayarisha, watawala wanashauriana pamoja kumwasi Yawe na muchaguliwa wake.


“Nimemusimika mufalme niliyemuchagua; anatawala Sayuni, mulima wangu mutakatifu!”


Yawe ni rafiki ya wale wanaomwabudu; yeye anawajulisha agano lake.


Roho wa Bwana wetu Yawe yuko pamoja nami, maana Yawe amenichagua, akanituma niwahubirie wanaoteswa habari njema, niwatunze waliovunjika moyo, niwatangazie waliohamishwa kwamba watapata uhuru, na wafungwa kwamba watafunguliwa.


Hakika, Bwana wetu Yawe hafanyi kitu bila kuwafunulia watumishi wake manabii nia yake.


Nyuma ya maneno haya, Mungu akawaonya katika ndoto kwamba wasirudie tena kwa Herode, kisha wakarudia katika inchi yao wakipitia njia nyingine.


“Sasa, Ee Bwana, umuruhusu mutumishi wako akufe katika amani, maana umetimiza ahadi yako.


Kweli ninawaambia: wamoja kati ya watu wanaokuwa hapa hawatakufa mbele ya kuona Ufalme wa Mungu unasimama.”


Andrea alimukuta kwanza Simoni, ndugu yake wa tumbo na kumwambia: “Tumemwona Masiya” (maana yake “Kristo”).


Lakini hii imeandikwa kusudi mupate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mupate uzima katika jina lake.


“Mukuje mumwone mutu aliyeniambia maneno yote niliyotenda. Huyu si Kristo?”


Kweli, kweli ninawaambia: kama mutu akishika maneno yangu, hatakufa hata milele.”


Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.


Aliwaelezea na kuwaonyesha wazi kwamba Kristo alipaswa kuteswa na kufufuka. Akawaambia: “Huyu Yesu ninayemuhubiri kwenu ndiye Kristo.”


“Kwa hiyo watu wa taifa la Israeli wajue hakika kwamba yule Yesu muliyemutundika juu ya musalaba, Mungu amemufanya kuwa Bwana na Masiya!”


Na bila kukawia akaanza kuhubiri katika nyumba za kuabudia, akitangaza kwamba Yesu ni Mwana wa Mungu.


Kwa njia ya imani, Enoki alibebwa na Mungu toka katika dunia pasipo kufa. Naye hakuonekana tena, kwa sababu Mungu alimubeba mbinguni. Maana Maandiko Matakatifu yanasema kwamba mbele ya kubebwa kwake, Enoki alishuhudiwa kwamba alimupendeza Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ