16 Halafu wakaenda kwa haraka, wakawakuta Maria, Yosefu na mutoto amelalishwa katika sanduku ya kukulishia nyama.
Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.
Katika siku zile, Maria akafunga safari, akaenda kwa haraka katika muji mumoja uliokuwa katika vilima vya Yudea.
Basi wale waliotumwa wakaenda, wakakuta vyote kama vile Yesu alivyowaambia.
Na hiki ndicho kitambulisho kwenu: mutamukuta mutoto muchanga amefunikwa nguo za kitoto, naye amelalishwa katika sanduku ya kukulishia nyama.”
Wale wamalaika walipoondoka na kurudia mbinguni, wachungaji wakasemezana: “Basi tuende Betelehemu, kusudi tupate kuona jambo lile lililotokea, ambalo Bwana alitujulisha.”
Nao walipokwisha kumwona mutoto huyo muchanga, wakaeleza maneno waliyoambiwa na malaika juu yake.
Akazaa mwana, ndiye muzaliwa wake wa kwanza. Akamufunika nguo za kitoto na kumulalisha katika sanduku ya kukulishia nyama, kwa sababu walikosa nafasi ya kukaa katika nyumba ya kupangisha wageni.
Wakaenda na kukuta vitu vyote sawa vile Yesu alivyowaambia. Nao wakatayarisha karamu ya Pasaka.