Muimbe kwa furaha enyi mbingu, kwa sababu ya yale Yawe aliyotenda. Mupige kelele enyi vilindi vya dunia! Mupige vigelegele enyi milima! Enyi mapori na miti yote inayokuwa ndani yake, mushangilie. Maana Yawe amewakomboa wazao wa Yakobo, naye atatukuzwa katika inchi ya Israeli.
Muimbe kwa furaha, enyi mbingu! Ushangilie ewe dunia, Enyi milima, mulalamike kwa furaha, maana Yawe amewafariji watu wake, anawaonea huruma watu wake wanaoteseka.
Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria, na kuirizi inchi ya Nimurodi. Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria, watakapoingia katika inchi yetu na kuanza kuishambulia.
Nalo kundi la watu waliomutangulia Yesu na lile la watu waliofuata nyuma yake, wakaanza kulalamika, wakisema: “Usifiwe wewe Mwana wa Daudi! Abarikiwe huyu anayekuja kwa jina la Bwana! Mungu asifiwe juu mbinguni!”
na Roho Mutakatifu akashuka juu yake katika hali ya kimwili kwa mufano wa njiwa. Na sauti ikasikilika toka mbinguni ikisema: “Wewe ndiwe Mwana wangu mupendwa; ninapendezwa nawe sana.”
Sasa kufuatana na vile tumekwisha kuhesabiwa haki mbele ya Mungu kwa njia ya imani, kunakuwa sasa amani kati yetu na Mungu kwa njia ya Bwana wetu Yesu Kristo.
Kwa njia ya Mwana wake alitaka kupatanisha ulimwengu muzima naye. Kwa njia ya damu ya Mwana wake iliyomwangika juu ya musalaba, Mungu ameleta amani, hivi akapatanisha vitu vyote naye mwenyewe, vinavyokuwa katika dunia na katika mbingu.
Nikasikia vilevile viumbe vyote vinavyokuwa mbinguni, katika dunia, katika kuzimu na vile vinavyokuwa katika bahari; viumbe vyote vya ulimwengu nzima vikimwimbia: “Utukufu, heshima, sifa na nguvu milele na milele, kwa yule anayeikaa juu kiti cha kifalme na kwa Mwana-Kondoo.”