Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 2:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Leo hii Mwokozi amezaliwa kwa ajili yenu katika muji wa Daudi, yeye ndiye Kristo na Bwana.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 2:11
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Fimbo ya kifalme haitatoka kwa Yuda, wala bakora ya utawala kwenye miguu yake, mpaka atakapofika yule ambaye ni yake; ambaye mataifa yatamutii.


Wafalme wa dunia wanajitayarisha, watawala wanashauriana pamoja kumwasi Yawe na muchaguliwa wake.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Yeye atazaa mutoto mwanaume, nawe utamwita jina lake Yesu, kwa maana ndiye atakayewaokoa watu wake toka katika zambi zao.”


Simoni Petro akamujibu: “Wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu Mwenye Uzima.”


Kisha Yesu akawakataza sana wanafunzi wake wasimwambie mutu kwamba yeye ndiye Kristo.


Namna gani nimepata bahati hii ya kutembelewa na mama ya Bwana wangu?


Ametuletea Mwokozi mwenye uwezo, toka ukoo wa mutumishi wake Daudi.


alikuwa amemufunulia kwamba hatakufa mbele hajamwona Kristo wa Bwana.


Basi Yosefu naye vilevile akaondoka katika muji Nazareti, wa jimbo la Galilaya, na kwenda Yudea katika muji wa kuzaliwa wa mufalme Daudi, unaoitwa Betelehemu. Alienda kule kwa sababu alikuwa mutu wa ukoo wa Daudi.


Andrea alimukuta kwanza Simoni, ndugu yake wa tumbo na kumwambia: “Tumemwona Masiya” (maana yake “Kristo”).


Kisha Filipo akamukuta Natanaeli, akamwambia: “Tumemwona yule ambaye Musa aliandika habari zake katika kitabu cha Sheria na ambaye manabii walisema juu yake. Ni Yesu wa Nazareti, mwana wa Yosefu.”


Akamujibu: “Ndiyo, Bwana, ninaamini kwamba wewe ni Kristo, Mwana wa Mungu, yule aliyepaswa kuja katika dunia.”


Lakini hii imeandikwa kusudi mupate kuamini kwamba Yesu ni Kristo, Mwana wa Mungu, na kwa kumwamini mupate uzima katika jina lake.


Mwanamuke yule akamwambia: “Ninajua kwamba Masiya anayeitwa Kristo, atakuja. Na wakati atakapokuja atatuelezea maneno yote.”


nao wakamwambia yule mwanamuke: “Sasa tunaamini, si kwa sababu ya maneno uliyotuambia tu, lakini kwa sababu tumesikia sisi wenyewe na tunajua hakika kwamba huyu ni Mwokozi wa dunia.”


Na sasa tunaamini na kujua kwamba wewe ni Mutakatifu wa Mungu.”


Wengine wakasema: “Huyu ni Kristo.” Lakini wengine wakasema: “Basi Kristo angeweza kutokea Galilaya?


Yeye ametuma ujumbe wake kwa Waisraeli, akiwahubiri Habari Njema ya amani kwa njia ya Yesu Kristo, anayekuwa Bwana wa watu wote.


Na toka katika uzao wa mutu huyo Mungu akawaletea Waisraeli Mwokozi, ndiye Kristo, kama vile alivyokuwa amewaahidia.


Aliwaelezea na kuwaonyesha wazi kwamba Kristo alipaswa kuteswa na kufufuka. Akawaambia: “Huyu Yesu ninayemuhubiri kwenu ndiye Kristo.”


“Kwa hiyo watu wa taifa la Israeli wajue hakika kwamba yule Yesu muliyemutundika juu ya musalaba, Mungu amemufanya kuwa Bwana na Masiya!”


Mungu alimupa utukufu na kumwikalisha na mamlaka karibu naye na kumuweka kuwa Mutawala na Mwokozi. Na hivi Waisraeli wataweza kugeuka toka zambi zao na Mungu atawasamehe.


Adamu wa kwanza aliumbwa kwa udongo, yeye ni wa dunia, lakini Adamu wa pili alitoka mbinguni.


na kila mutu akubali kwamba Yesu ni Bwana, naye Mungu Baba atatukuzwa kwa njia hiyo.


Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo


Basi kwa sababu mumemukubali Kristo kuwa Bwana wenu, muishi katika kuungana naye.


Na sisi tumeona na kushuhudia kwamba Baba amemutuma Mwana wake kuwa Mwokozi wa dunia.


Mutu yeyote anayeamini kwamba Yesu ndiye Kristo, yeye ni mutoto wa Mungu; na kila mutu anayemupenda baba anamupenda mwana wake vilevile.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ