Katika mwaka wa kumi na tano wa utawala wa Tiberio mufalme wa Roma, Pontio Pilato alikuwa liwali wa jimbo la Yudea, na Herode alikuwa mutawala wa jimbo la Galilaya na ndugu yake Filipo alikuwa mutawala wa inchi ya Iturea na ya Tarakoniti. Vilevile Lisania alikuwa mutawala wa inchi ya Abilene,
Na mumoja wao, aliyeitwa Agabo, akasimama, akatabiri kwa njia ya Roho Mutakatifu kwamba kutakuwa njaa kubwa katika dunia nzima. (Nayo ikatokea katika nyakati za utawala wa mufalme Klaudio wa Roma.)
Kama mimi ni mukosaji au nimefanya kitendo kinachonipasa kuuawa, mimi sikatai kufa. Lakini kama hakuna ukweli wowote katika mashitaki yao juu yangu, hakuna mutu anayeweza kunitoa kwao. Ninaomba kusambishwa na Mufalme wa Roma.”