40 Yesu akawajibu: “Ninawaambia ninyi: kama watu hawa wakinyamaza, mawe yatalalamika.”
Mufurahi, enyi mbingu na dunia! Bahari ivume pamoja na vyote vinavyokuwa ndani yake!
Mutatoka Babeli kwa furaha; mutaongozwa muende kwa amani. Milima na vilima mbele yenu vitapiga kelele na kuimba, na miti yote katika mashamba itawapigia mikono.
Ndiyo maana hata mawe yatalalamika juu ya ukuta, na miti ya nyumba itayaunga mukono.
Tangia saa sita ya muchana, giza lilikuwa katika inchi yote mpaka saa tisa.
Musijifikiri kwamba munaweza kujidai tu kuwa Abrahamu ndiye babu yenu. Ninawaambia kwamba Mungu anaweza kugeuza mawe haya kuwa watoto wa Abrahamu!
Yesu alipokaribia muji wa Yerusalema, na alipouona, akaulilia,
Vilevile Mungu alihukumu muji wa Sodoma na Gomora na kuiteketeza kwa moto. Kwa njia hiyo, alionyesha mufano wa mambo yatakayotokea kwa watu waovu.