42 Yesu akamwambia: “Upate kuona! Imani yako imekuponyesha.”
Kwa neno lake aliwaponyesha, akawaokoa wasiangamie.
Maana alisema, na ulimwengu ukakuwa; alitoa amri, nao ukajitokeza.
Halafu Yesu akamujibu: “Wewe mwanamuke, imani yako ni kubwa! Ifanyike kwako sawa ulivyoomba.” Na binti yake akapona tangia saa ile ile.
Yesu akanyoosha mukono, akamugusa na kumwambia: “Ninataka, utakaswe!” Na mara moja mutu yule akatakaswa ukoma wake.
Naye Yesu alipogeuka, akamwona na kumwambia: “Binti yangu, ujipe moyo! Imani yako imekuponyesha.” Na mwanamuke yule akapona saa ile ile.
Kisha Yesu akamwambia mutu yule: “Simama, ujiendee. Imani yako imekuponyesha.”
“Unataka nikufanyie nini?” Akamujibu: “Bwana, ninataka nipate kuona.”
Lakini Yesu akamwambia tena yule mwanamuke: “Kwenda na amani, imani yako imekuokoa.”
Na Yesu akamwambia: “Binti yangu, imani yako imekuponyesha. Ujiendee na amani.”