Lakini akamujibu baba yake: ‘Ninakutumikia kwa miaka mingi na sijakukosea hata mara moja. Ingawa vile haujanipatia hata kitoto cha mbuzi kusudi nifurahi pamoja na warafiki zangu.
Vilevile ninawaambia, ndivyo kutakuwa furaha kubwa zaidi mbinguni kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake, kuliko wenye haki makumi tisa na tisa wasiokuwa na lazima ya kugeuka toka zambi zao.
Yesu aliposikia maneno haya, akamwambia: “Ungali unakosewa na kitu kimoja tu: uuzishe vitu vyote unavyokuwa navyo, na uwape wamasikini mali zile, nawe utakuwa na akiba mbinguni. Kisha urudie unifuate!”