Luka 18:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
16 Lakini Yesu akawaita na kusema: “Muwaache watoto wadogo wakuje kwangu, wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa Mungu ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.
Lakini Yesu akawaambia wanafunzi wake: “Muwaache watoto wakuje kwangu, wala musiwakataze, kwa maana Ufalme wa mbinguni ni wa watu wanaokuwa sawasawa na wao.”
Wandugu zangu, musikuwe kama watoto kwa kufikiri: lakini katika mambo mabaya, iwatokee kutenda kama watoto wachanga. Inafaa mafikiri yenu yakuwe kama ya watu wazima.
Kwa maana, mume asiyeamini anapata ushirika na Mungu kwa njia ya kuungana kwake na muke wake. Vilevile muke asiyeamini anapata ushirika na Mungu kwa njia ya kuungana kwake na mume wake. Kama isingekuwa vile, watoto wao wangehesabiwa kama watoto wa wapagani, lakini kwa hakika wao ni watu wa Mungu.
Mutakusanya wanaume, wanawake, watoto na wageni wanaoishi katika miji yenu, kusudi kila mumoja asikie maneno haya ya kujifunza kumwogopa Yawe, Mungu wenu, na kuwa waangalifu kushika maneno ya sheria hii.