Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 17:30 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

30 Ni hivi itakavyokuwa siku ile Mwana wa Mutu atakayotokea.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 17:30
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa maana Mwana wa Mutu atakuja na wamalaika akitukuzwa na Baba yake, halafu atamulipa kila mutu kufuatana na matendo yake.


Basi Yesu alipokuwa akiikaa kwa mulima wa Mizeituni, wanafunzi wake wakamwendea peke yao na kumwuliza: “Utuambie, mambo hayo uliyotoka kusema yatakuwa wakati gani? Na kitambulisho cha kurudi kwako nao wakati wa mwisho wa dunia ni nini?”


Kama ilivyokuwa katika siku za Noa, ndivyo itakavyokuwa wakati Mwana wa Mutu atakaporudi.


Nao hawakutambua kitu mpaka mvua kubwa sana ilipotokea, na kuwaua wote. Na ni hivi itakavyokuwa wakati Mwana wa Mutu atakaporudi.


Yesu akamujibu: “Wewe umesema. Lakini zaidi ya hiyo, ninawaambia ninyi kwamba mutamwona Mwana wa Mutu akiikaa na mamlaka karibu na Mungu Mwenye Uwezo. Mutamwona vilevile akikuja katika mbingu katikati ya mawingu!”


Na halafu wakati ule Mwana wa Mutu ataonekana akikuja katikati ya mawingu kwa uwezo mwingi na kwa utukufu.


Kwa maana kama vile umeme unavyoangaza na kuonekana wazi katika mbingu yote, ni vile Mwana wa Mutu atakavyoonekana siku atakapokuja.


Lakini siku ile Loti alipoondoka Sodoma, moto na kiberiti vikashuka kama mvua toka mbinguni na kuwaangamiza wote.


Kwa maana siku zile zitakuwa siku za azabu ya Mungu, kusudi mambo yote yaliyoandikwa katika Maandiko Matakatifu yatimie.


Halafu wakati ule Mwana wa Mutu ataonekana akikuja katikati ya mawingu, kwa uwezo mwingi na kwa utukufu.


hata hamukosewi zawadi yoyote ya Mungu, mukiwa mukingojea wakati Bwana wetu Yesu Kristo atakapoonekana.


Ni yeye atakayewasimamisha ninyi imara mpaka mwisho kusudi musishitakiwe juu ya kosa lolote Siku ile ya kurudi kwa Bwana wetu Yesu Kristo.


Kristo ndiye uzima wenu wa kweli, naye atakapoonekana tena, basi ninyi mutaonekana pamoja naye katika utukufu wake.


na kuwapumzisha ninyi munaoteswa pamoja nasi. Jambo lile litatendeka wakati Bwana Yesu atakapoonekana tokea mbinguni pamoja na wamalaika wake wenye uwezo,


Kwa sababu hiyo, mukuwe tayari kwa kutumikisha akili yenu. Mukeshe na muweke tumaini lenu lote katika baraka ile mutakayopewa wakati Yesu atakapotokea.


Majaribu hayo ni kwa ajili ya kupima imani yenu. Zahabu ni kitu kinachoharibika, lakini ingawa vile inapimwa kwa njia ya kuchomwa ndani ya moto. Hivi vilevile imani yenu inayokuwa ya bei kali kuliko zahabu, inapaswa kupimwa kusudi ijulikane kuwa ya kweli. Na kwa sababu hii mutapata sifa, utukufu na heshima wakati Yesu Kristo atakapotokea.


Lakini mufurahi kwa sababu munashiriki katika mateso ya Kristo. Na kwa hiyo mutashangilia kwa furaha wakati atakapoonekana katika utukufu.


Na sasa watoto wangu, mukae ndani yake kusudi tukuwe na tumaini hakika wakati atakapotokea, na kutosikia haya mbele yake siku atakaporudi.


Wapendwa wangu, sasa sisi ni watoto wa Mungu, wala namna tutakavyokuwa haijaonekana bado waziwazi. Lakini tunajua kwamba wakati Kristo atakapotokea, tutafanana naye kwa sababu tutamwona vile anavyokuwa.


Angalia, yeye anakuja katikati ya mawingu! Kila mutu atamwona, hata wale waliomutoboa kwa mukuki. Na kwa sababu yake mataifa yote ya dunia yatalalamika kwa huzuni. Hakika ni vile! Amina.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ