Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 16:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Basi bwana wa yule mulinzi akamusifu kwa sababu alitenda kwa werevu. Kwa maana watu wa dunia hii wanatengeneza maneno yao na wenzao kwa werevu sana kuliko watu wanaopenda kuishi katika mwangaza.”

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 16:8
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nyoka alikuwa mwerevu kuliko nyama wote wa pori walioumbwa na Yawe Mungu. Basi, nyoka akamwambia yule mwanamuke: “Ni kweli Mungu alisema musikule matunda ya muti wowote katika bustani?”


Lakini Amunoni alikuwa na rafiki aliyeitwa Yonadabu, mwana wa Shama, ndugu ya Daudi. Yonadabu alikuwa mutu mwerevu sana.


Uwaite manabii wote wa Bali, wafuasi wake wote na makuhani. Ni sharti kila mumoja afike, maana ninataka kumutolea Bali sadaka kubwa, na yeyote atakayekosa kufika atauawa.” Hiyo ilikuwa ni namna ya Yehu ya kudanganya kusudi apate kuwaua wafuasi wa Bali.


Ee Yawe, mukono wako uwafukuze kati ya watu, tukio lao likuwe kutengana na wanaokuwa wazima. Uwashibishe kwa akiba uliyowawekea, watoto wao nao washibe na kuacha sehemu, wawaachie hata na wajukuu wao.


Ni lazima tutafute werevu wa kuwapunguza na kuzuia wasiongezeke; kama sivyo, vita ikitokea watajiunga na waadui zetu na kutoroka inchi.”


Mutu anasifiwa kadiri ya hekima yake, lakini mwenye moyo wa mafikiri mabaya anazaruliwa.


Kila mutu anayesema vibaya juu ya Mwana wa Mutu atasamehewa, lakini kila mutu anayesema vibaya juu ya Roho Mutakatifu, hatasamehewa katika ulimwengu huu, wala katika ule unaokuja.


Petro akamujibu: “Watu wengine.” Na Yesu akamwambia: “Basi ni kusema kwamba watu wa jamaa zao wako na ruhusa ya kutolipa.


Yule anayekuwa mwaminifu katika vitu vichache, yuko mwaminifu vilevile katika vitu vingi. Na yule asiyekuwa mwaminifu katika vitu vichache, hayuko mwaminifu vilevile katika vitu vingi.


Sasa ninajua jinsi nitakavyofanya kusudi wakati nitafukuzwa kwa kazi yangu ya ulinzi, watu wapate kunikaribisha katika nyumba zao.’


Kisha akamwuliza mwingine: ‘Na wewe uko na deni yapata gani?’ Naye akajibu: ‘Saki mia moja za ngano.’ Yule mulinzi akamwambia: ‘Kamata barua yako ya mapatano na uandike saki makumi nane.’


Halafu Bwana akasema: “Musikilize jinsi mwamuzi huyu mubaya anavyosema!


Yesu akawajibu: “Watu wa nyakati hizi wanaoa na kuolewa.


Lakini wale watakaohesabiwa kwamba wanastahili kufufuliwa na kuishi katika nyakati zile zitakazokuja, hawataoa wala kuolewa.


Basi muaminie mwangaza ule wakati mungali nao, kusudi mukuwe watu wa mwangaza.” Yesu alipokwisha kusema maneno hayo, akajiendea na kujificha mbali na lile kundi.


Mutu yeyote asijidanganye mwenyewe. Kama mutu fulani kati yenu akijizania kuwa mwenye hekima ya kidunia, ajifanye kama mupumbafu kusudi apate kuwa na hekima ya kweli.


Zamani muliishi katika giza, lakini sasa, kwa kuungana kwenu na Bwana, munaishi katika mwangaza. Muishi kama watoto wa mwangaza,


Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.


Kwa maana ninyi wote ni watu wanaoishi katika mwangaza, ndio watu wa muchana. Sisi si watu wa usiku wala wa giza.


Lakini ninyi ni watu wa kizazi kilichochaguliwa na Mungu na wa ukuhani wa kifalme. Ninyi ni taifa takatifu na watu wa pekee wa Mungu. Mumechaguliwa kusudi mutangaze matendo makubwa ya yule aliyewaita kutoka katika giza na kuwaingiza kwenye mwangaza wake wa ajabu.


Hii ndiyo njia inayoonyesha wazi tofauti kati ya watoto wa Mungu na watoto wa Shetani. Mutu asiyetenda mambo ya haki au asiyemupenda ndugu yake si mutoto wa Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ