Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 16:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Yule mulinzi akajiuliza: ‘Sasa nitafanya nini? Bwana wangu ananifukuza kwa kazi. Kulima, mimi siwezi; na kuombaomba, ninasikia haya.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 16:3
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hamani alipoingia ndani, mufalme akamwuliza: “Nimufanyie nini mutu ambaye ningependa sana kumupatia heshima?” Hamani akafikiri ndani ya moyo wake: “Ni nani huyo ambaye mufalme angependa kumupatia sana heshima? Bila shaka ni mimi.”


Muvivu anatamani lakini hapati kitu chochote, wakati mwenye bidii anajaliwa kwa wingi.


Njia ya muvivu inajaa miiba, lakini njia ya mutu wa usawa ni wazi kama barabara kubwa.


Mutu muvivu katika kazi yake ni ndugu ya muharibifu.


Uvivu ni kama usingizi muzito; mutu muvivu atateseka kwa njaa.


Muvivu halimi wakati wa kulima; wakati wa mavuno atatafuta lakini hatapata kitu.


Anayebembeleza mutumwa wake tangu utoto, kwa mwisho mutumwa yule atamurizi.


Mutafanya nini siku ya azabu, siku zoruba itakapowakujia kutoka mbali? Mutamukimbilia nani kwa kuomba musaada? Mutakwenda wapi kwa kuweka mali yenu?


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Mutafanya nini katika sikukuu ile iliyopangwa, au katika karamu ya Yawe?


“Ilipokuwa magaribi, mwenye shamba akamwambia musimamizi wake: ‘Uwaite watumishi na uwalipe mushahara wao, ukianzia kwa wale wa mwisho mpaka kwa wale wa kwanza.’


Wakafika Yeriko. Na wakati Yesu alipokuwa akitoka kule pamoja na wanafunzi wake na kundi kubwa la watu, mutu mumoja kipofu aliyeitwa Bartimayo mwana wa Timayo, alikuwa akiikaa pembeni ya njia akiombaomba.


Yeye akawaza na kusema: ‘Nitafanya nini hivi ninakosewa nafasi ya kuwekea mavuno yangu yote?’


Halafu bwana wake akamwita na kumwambia: ‘Ni habari gani ile waliyonielezea juu yako? Ninakuomba unifanyie hesabu yote ya mali yangu, kwa sababu hauwezi tena kuwa mulinzi wa mali yangu.’


Vilevile kulikuwa masikini mumoja aliyeitwa Lazaro aliyekuwa na vidonda mwili wote, alibaki akilala mbele ya mulango wa nyumba ya yule tajiri.


Siku moja yule masikini akakufa, na wamalaika wakamupeleka mpaka pembeni ya Abrahamu. Na yule tajiri akakufa vilevile na kuzikwa.


Sasa ninajua jinsi nitakavyofanya kusudi wakati nitafukuzwa kwa kazi yangu ya ulinzi, watu wapate kunikaribisha katika nyumba zao.’


Kwa muda murefu yule mwamuzi alikataa. Lakini kisha akajiuliza mwenyewe: ‘Ijapokuwa mimi simwogopi Mungu wala simujali mutu yeyote,


Jirani zake na wale waliomwona zamani akiwa mwenye kuombaomba, wakasema: “Si mutu huyu ndiye yule aliyekuwa akiikaa chini na kuombaomba?”


Karibu na mulango mumoja wa hekalu unaoitwa “Muzuri,” kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa kiwete tangia kuzaliwa kwake. Kila siku walimubeba na kumuweka kwenye mulango huo kusudi aombe musaada kwa watu waliokuwa wakiingia katika hekalu.


Lakini simama, uingie katika muji, na mule watakuambia jambo unalopaswa kufanya.”


Tunasema hivi kwa sababu tumepata habari kwamba wamoja kati yenu ni wavivu; hawatumiki, isipokuwa tu kujiingiza katika maneno ya wengine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ