Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 16:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 kwa maana niko na wandugu watano. Aende kuwaonya, kusudi nao vilevile wasikuje katika nafasi hii ya mateso.’

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 16:28
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu tajiri akasema: ‘Basi, baba ninakuomba umutume Lazaro kwa nyumba ya baba yangu,


Akatuagiza kutangaza Habari Njema kwa watu na kushuhudia kwamba ni yeye aliyewekwa na Mungu kuwa Mwamuzi wa wazima na wafu.


Sila na Timoteo walipofika toka Makedonia, Paulo akajitolea sana kwa kuhubiri Neno la Mungu, akihakikisha kwa Wayuda kwamba Yesu ndiye Kristo.


Petro akazidi kusema maneno mengine ya kuwaonya na kuwatia moyo, akisema: “Mujiokoe toka kati ya kizazi hiki kipotovu!”


Nimewaonya Wayuda wa mataifa mengine kwamba wanapaswa kumugeukia Mungu na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo.


Lakini kitu kimoja ninachojua tu, ni kwamba katika kila muji Roho Mutakatifu ananihakikishia kwamba vifungo na mateso vinaningojea.


Lakini sihesabu maisha yangu kuwa kitu cha bei kali kwangu. Shabaha moja ninayokuwa nayo ni kufikia mwisho wa utumishi wangu na kutimiza kazi ile niliyopewa na Bwana Yesu; maana yake kushuhudia Habari Njema ya neema ya Mungu.


Usiku ule ule Bwana akamutokea Paulo, akamwambia: “Ujipe moyo! Sawa vile ulivyotoa ushuhuda juu yangu hapa Yerusalema, ni vile vile utakavyopaswa kuutoa katika Roma.”


Lakini kwa ulinzi wa Mungu ningali muzima hata leo. Nami ninatoa ushuhuda kwa wadogo na wakubwa, wala sisemi maneno mengine yanayokuwa mbali na yale manabii na Musa waliyosema kwamba yatatokea.


Halafu wakapanga siku ya kukutana na Paulo. Na siku ile watu wengi zaidi wakamufikia pahali alipopanga. Na tangu asubui mpaka magaribi Paulo akawaelezea mambo mengi na kutoa ushuhuda juu ya habari za Ufalme wa Mungu. Alitaka wasadiki habari za Yesu akitaja maneno ya Sheria ya Musa na ya vitabu vya manabii.


Kisha kushuhudia na kuhubiri neno la Bwana, Petro na Yoane wakarudi Yerusalema wakitangaza Habari Njema katika vijiji vingi vya Samaria.


Mimi ninasema tena wazi, kila mutu anayekubali kutahiriwa sherti ashike Sheria yote.


Basi, kwa jina la Bwana ninawaonya hivi: musiishi tena kama watu wa mataifa mengine, wanaofuata mawazo yao ya bure


Munajua vizuri kwamba tulimutendea kila mumoja wenu kama vile baba anavyowatendea watoto wake mwenyewe.


Kuelekea maneno hayo, mutu yeyote asimukosee ndugu yake wala kumudanganya. Tumekwisha kuwaambia na kuwahakikishia mbele kwamba Bwana atawaazibu wale wanaofanya mambo kama hayo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ