Tokea kwenye muguu mpaka kwenye kichwa hakuna chenye kuwa kizima; ni machubuko, alama za mapigo na vidonda vinavyovuja damu, vilivyokosa kusafishwa, kufungwa wala kutulizwa kwa mafuta.
Petro alipotoka inje kwa mulango wa upango, mutumishi mwingine mwanamuke akamwona na kuwaambia wale waliokuwa pale: “Huyu alikuwa pamoja na Yesu wa Nazareti.”
Karibu na mulango mumoja wa hekalu unaoitwa “Muzuri,” kulikuwa mutu mumoja aliyekuwa kiwete tangia kuzaliwa kwake. Kila siku walimubeba na kumuweka kwenye mulango huo kusudi aombe musaada kwa watu waliokuwa wakiingia katika hekalu.
Wandugu zangu wapenzi, musikilize: Mungu amewachagua wamasikini wa dunia hii kusudi wakuwe watajiri katika imani, nao wapokee Ufalme ule aliowaahidi wale wanaomupenda.
Anawainua wazaifu toka katika mavumbi, anawanyanyua wakosefu toka katika majivu, na kuwaikalisha pamoja na wakubwa, na kuwarizisha viti vya heshima. Maana, minara ya dunia ni ya Yawe; yeye ameisimika dunia juu ya minara yake.