Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 16:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Halafu bwana wake akamwita na kumwambia: ‘Ni habari gani ile waliyonielezea juu yako? Ninakuomba unifanyie hesabu yote ya mali yangu, kwa sababu hauwezi tena kuwa mulinzi wa mali yangu.’

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 16:2
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Maana, Mungu atahukumu matendo yote, hata yale yanayotendwa kwa siri, yakuwe mazuri au mabaya.


“Ninawaambia wazi kwamba kwa Siku ya hukumu, watu watasamba kila neno lisilokuwa na maana walilosema.


“Ilipokuwa magaribi, mwenye shamba akamwambia musimamizi wake: ‘Uwaite watumishi na uwalipe mushahara wao, ukianzia kwa wale wa mwisho mpaka kwa wale wa kwanza.’


Lakini Mungu akamwambia: ‘Mupumbafu wewe! Leo leo usiku utakufa. Na sasa, vitu hivi vyote ulivyojitayarishia vitakuwa vya nani?’ ”


Bwana akajibu: “Ni nani basi anayekuwa musimamizi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kwa kuwasimamia watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho lao kwa wakati uliopangwa.


Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu: “Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyekuwa na mulinzi wa mali yake. Yule mulinzi akachongewa kwa bwana wake kwamba anaponda mali yake.


Yule mulinzi akajiuliza: ‘Sasa nitafanya nini? Bwana wangu ananifukuza kwa kazi. Kulima, mimi siwezi; na kuombaomba, ninasikia haya.


Kwa hiyo kila mumoja kati yetu atajitetea mwenyewe kwa Mungu.


Kwa maana, wandugu zangu, nimepata habari zenu kwa njia ya jamaa ya Kloe kwamba kuko ugomvi katikati yenu.


Yanayohitajika kwa mwenye madaraka kama hayo, ni kuwa mwaminifu.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Kwa maana sisi wote tunapaswa kusimama kwa kusambishwa mbele ya tribinali ya Kristo, kusudi kila mutu alipwe kufuatana na matendo yake mema au mabaya aliyofanya alipokuwa akiishi ndani ya mwili wake.


Usiache kutumia ile zawadi ya kiroho inayokuwa ndani yako, uliyopokea kutokana na maneno ya manabii na kwa njia ya kuwekewa mikono na wazee wa kanisa.


Zambi za watu wamoja zinaonekana waziwazi hata mbele hawajahukumiwa. Lakini zambi za wengine zinajulikana kisha.


Kila mutu kati yenu anapaswa kuitumia zawadi ya kiroho aliyojaliwa na Mungu kwa ajili ya mafaa ya wengine. Na hivi mutakuwa walinzi wazuri wa zawadi mbalimbali mulizopewa na Mungu.


Lakini watu hawa watasamba maneno yao mbele ya Mungu anayekwisha kuwa tayari kwa kuhukumu wafu na wazima.


Nikaona wale waliokufa, wakubwa na wadogo wakisimama mbele ya kile kiti cha kifalme. Vitabu vikafunguliwa na kitabu kingine kikafunguliwa ndicho kitabu cha uzima. Wale waliokufa wakahukumiwa kufuatana na matendo yao sawa vile ilivyoandikwa katika vitabu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ