Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 16:19 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

19 “Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyezoea kuvaa nguo zenye kuwa laini sana za bei kali zaidi na aliyeishi katika raha siku zote.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 16:19
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mordekayi alipotoka katika nyumba kwa mufalme, akiwa amevaa nguo ya kifalme ya rangi ya mayungiyungi na nyeupe, koti la kitani safi la rangi nyekundu, na taji kubwa ya zahabu, muji wa Susani ukajaa shangwe na vigelegele.


Mali ni taji ya utukufu wa wenye hekima, lakini ujinga ni kitambaa cha wapumbafu.


Anajitengenezea matandiko, nguo zake ni za rangi nyeusi-nyekundu za kitani safi.


nguo nzuri, shemizi nzuri, vioo na vitambaa mbalimbali.


Basi, ukapambwa kwa zahabu na feza. Nguo yako ikakuwa ya kitani safi na hariri, nayo ilikuwa imepambwa. Ulitumia unga safi, asali na mafuta kwa chakula chako. Ukakuwa na sura nzuri sana, ukaifikia hali ya malkia.


Kosa la dada yako Sodoma, lilikuwa hili: yeye pamoja na wabinti wake walipokuwa na chakula nao walifanikiwa sana, walianza kujivuna, wakaacha kuwasaidia wamasikini na wakosefu.


Kitani kilichopindwa vizuri kutoka Misri kilikuwa kwa kupamba tanga lako na kwa ajili ya bendera yako. Chandarua chako kilitengenezwa na nguo ya rangi ya samawi na nyekundu-nyeusi kutoka visanga vya Elisa.


Wakamuvalisha Yesu nguo nyekundu, na wakasokota taji na tawi lenye miiba na kumuvalisha nalo juu ya kichwa.


Walipokwisha kumuchekelea, wakamuvua ile nguo nyekundu na kumuvalisha nguo zake. Kisha wakaondoka naye inje kwa kwenda kumutundika juu ya musalaba.


Nyuma ya siku chache, yule mudogo akauzisha urizi wake na kwenda katika inchi ya mbali. Kule aliponda mali yake yote katika maisha ya ovyo.


Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu: “Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyekuwa na mulinzi wa mali yake. Yule mulinzi akachongewa kwa bwana wake kwamba anaponda mali yake.


“Kila mutu anayemufukuza muke wake na kuoa mwingine, anazini; na mutu anayemwoa yule muke aliyefukuzwa anazini vilevile.


Vilevile kulikuwa masikini mumoja aliyeitwa Lazaro aliyekuwa na vidonda mwili wote, alibaki akilala mbele ya mulango wa nyumba ya yule tajiri.


Yule mwanamuke alikuwa amevaa nguo za rangi nyekundunyeusi na nyekundu sana za bei kali, tena alikuwa amejipamba kwa zahabu, mawe ya bei kali na ushanga wa bei kali. Naye alikuwa anashika katika mukono wake kikombe kilichotengenezwa na zahabu chenye kujaa machukizo na mambo machafu ya uasherati wake.


wakisema: “Ole! Ole kwa muji ule mukubwa. Ulikuwa unavaa nguo zilizofumwa na nyuzi nzuri pamoja na nguo zuri ya rangi nyekundu nyeusi na nyekundu sana. Ulikuwa unapambwa kwa zahabu, mawe ya bei kali, na ushanga wa bei kali!


Na kwa kadiri ulivyojitukuza na kuishi katika raha, kwa kadiri ile ile muuletee mateso na huzuni. Muji ule unajisemesha: ‘Mimi ninaikaa juu ya kiti cha kifalme kama vile malkia; mimi si mujane, wala sitapata huzuni hata kidogo!’


Uzito wa pete zote alizoomba wamupe ulikuwa kilo makumi mbili. Zaidi ya hivyo, alipokea vilevile vyuma vya masikio, nguo za rangi nyekundu-nyeusi zilizovaliwa na wafalme wa Midiani na mikufu iliyokuwa kwenye shingo za ngamia wao.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ