Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 16:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Lakini ni vyepesi zaidi kwa mbingu na dunia kutoweka kuliko hata nukta moja ya Sheria kuondoshwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 16:17
11 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Majani yananyauka na maua yanafifia, lakini neno la Mungu wetu linadumu milele.


Muinue macho, muangalie mbingu, kisha muangalie dunia kule chini. Mbingu zitatoweka kama moshi, dunia itachakaa kama nguo, na wakaaji wake watakufa kama vidudu. Lakini wokovu ninaouleta unadumu milele; ukombozi wangu hautakoma hata kidogo.


Kweli ninawaambia: kwa muda wote mbingu na dunia vitakapokuwa vingali, hakuna hata herufi moja wala nukta moja ya Sheria itakayoondoshwa mpaka yote yatimie.


Mbingu na dunia vitatoweka, lakini maneno yangu hayatabadilika hata kidogo.


Basi ni kusema kwa sababu ya imani ile tunaitupilia Sheria? Hapana hata kidogo! Lakini tunasimamisha Sheria.


Lakini Neno la Bwana linadumu hata milele.” Na Neno hili ni Habari Njema iliyohubiriwa kwenu.


Siku Bwana atakaporudi, itatimia kama vile mwizi anavyokuja. Siku ile mbingu zitatoweka kwa shindo kubwa, na viumbe vyote vinavyoangaza katika mbingu vitayeyuka. Dunia na vitu vyote vinavyokuwa ndani yake vitateketezwa.


Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha kifalme pamoja na yule aliyeikaa juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele yake navyo havikuonekana tena.


Kisha nikaona mbingu mupya na dunia mupya. Kwa sababu mbingu ya kwanza na dunia ya kwanza vilikuwa vimekwisha kutoweka, bahari nayo haikukuwa tena.


Yeye atapanguza machozi yao yote na kifo hakitakuwa tena, wala kilio, wala malalamiko, wala maumivu. Kwa maana dunia ya mbele imekwisha kupita.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ