12 Na kama hamuwezi kulinda mali ya mutu mwingine kwa uaminifu, ni nani atakayewapa mali yenu ya pekee?
akisema: Nilikuja uchi katika dunia, nitaondoka uchi katika dunia. Yawe amenipa, Yawe ametwaa. Jina la Yawe litukuzwe.
Basi, nitafunga njia yake kwa miiba, nitamuzungushia ukuta, asipate njia ya kutokea inje.
Kuna kitu kimoja tu cha lazima. Maria amechagua kitu kinachokuwa kizuri zaidi ambacho hakuna mutu atakayekiondoa kwake.”
Basi kama ninyi hamukukuwa waaminifu kwa kulinda mali ya dunia hii, ni nani atakayeweza kuwatumainia kwa kulinda mali ya kweli?
“Hakuna mutumishi anayeweza kutumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kumutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.”