Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 16:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yesu akawaambia wanafunzi wake mufano huu: “Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyekuwa na mulinzi wa mali yake. Yule mulinzi akachongewa kwa bwana wake kwamba anaponda mali yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 16:1
19 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Abramu akasema: “Ee Yawe, utanipa nini wakati ninaendelea kuishi bila mutoto, na murizi wangu ni Eliezeri wa Damasiki?


Kwa hiyo wakamwendea yule musimamizi wa nyumba ya Yosefu wakaongea naye wakiwa kwa mulango,


Mufalme Daudi akakusanya kule Yerusalema wakubwa wote wa Waisraeli: wa makabila, majemadari na vikundi waliomutumikia mufalme, wakubwa wa maelfu na mamia, wasimamizi wa mali yote, ya ngombe wote wa mufalme na wana wake pamoja na wakubwa wa nyumba ya kifalme, mashujaa na waaskari wenye heshima.


Mutu muvivu katika kazi yake ni ndugu ya muharibifu.


Basi, nitafunga njia yake kwa miiba, nitamuzungushia ukuta, asipate njia ya kutokea inje.


“Ilipokuwa magaribi, mwenye shamba akamwambia musimamizi wake: ‘Uwaite watumishi na uwalipe mushahara wao, ukianzia kwa wale wa mwisho mpaka kwa wale wa kwanza.’


Bwana akajibu: “Ni nani basi anayekuwa musimamizi mwaminifu na mwenye akili? Ni yule bwana wake aliyemuweka kwa kuwasimamia watumishi wake wengine na kumwamuru kuwapatia posho lao kwa wakati uliopangwa.


Nyuma ya siku chache, yule mudogo akauzisha urizi wake na kwenda katika inchi ya mbali. Kule aliponda mali yake yote katika maisha ya ovyo.


Lakini mwana wako huyu aliyeharibu mali yako katika ukahaba alipofika, ukamuchinjia yule ngombe mwenye kunona!’


“Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyezoea kuvaa nguo zenye kuwa laini sana za bei kali zaidi na aliyeishi katika raha siku zote.


Halafu bwana wake akamwita na kumwambia: ‘Ni habari gani ile waliyonielezea juu yako? Ninakuomba unifanyie hesabu yote ya mali yangu, kwa sababu hauwezi tena kuwa mulinzi wa mali yangu.’


Kisha mutumishi mwingine akakuja akasema: ‘Bwana, furushi yako ndiyo hii. Niliichunga vizuri nikiifunga ndani ya kitambaa,


na Yoana muke wa Kuza, huyo mume wake alikuwa musimamizi wa mali ya Herode, pamoja na Suzana na wengine wengi. Wanawake hawa walitumia mali yao kwa kuwasaidia Yesu na wanafunzi wake.


Kwa maana musimamizi wa kanisa anapaswa kuwa mutu asiyeshitakiwa neno, kwa sababu yeye ni mwangalizi wa kazi ya Mungu. Hapaswi kuwa mutu mwenye kiburi, wala mukali, mulevi, mugomvi wala mwenye kutafuta mali kwa njia mbaya.


Wakati munapoomba, hamupati kitu kwa sababu munaomba kwa nia mbaya, kwa maana munataka vitu kusudi mutimize tu tamaa zenu.


Kila mutu kati yenu anapaswa kuitumia zawadi ya kiroho aliyojaliwa na Mungu kwa ajili ya mafaa ya wengine. Na hivi mutakuwa walinzi wazuri wa zawadi mbalimbali mulizopewa na Mungu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ