Vilevile ninawaambia, ndivyo kutakuwa furaha kubwa zaidi mbinguni kwa ajili ya mwenye zambi mumoja anayegeuka toka zambi zake, kuliko wenye haki makumi tisa na tisa wasiokuwa na lazima ya kugeuka toka zambi zao.
Mwenye bibi arusi ndiye bwana-arusi; lakini rafiki ya bwana arusi anasimama karibu naye na kumusikiliza, anafurahi sana kusikia sauti ya bwana-arusi. Na ni hivi mimi ninafurahi, na furaha yangu imetimia sasa.
Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote.
Kanisa liliwapatia vitu walivyohitaji kwa ajili ya safari ile, nao wakapita katika inchi ya Foinikia na katika Samaria. Na kule wakaeleza namna watu wa mataifa mengine walivyomugeukia Mungu. Habari hii ikafurahisha sana wandugu waamini wote.
Kwa hiyo wandugu zangu wapendwa, niko na hamu sana ya kuwaona tena. Ninyi ndio munaokuwa furaha yangu na zawadi ya ushindi nitakayopokea. Ninyi wapendwa wangu, ninawaomba musimame imara katika ushirika wenu na Bwana.