Muende kujifunza maana ya Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu.’ Kwa maana sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”
“Ni nani kati yenu akiwa na kondoo mia moja, na mumoja wao akipotea, atakayekosa kuwaacha wale wengine makumi tisa na tisa kwenye mashamba ya kulishia wanyama na kwenda kumutafuta yule aliyepotea mpaka atakapomupata?
Akamwuliza tena mara ya pili: “Simoni mwana wa Yoane, unanipenda?” Naye akamujibu: “Ndiyo, Bwana, unajua kama ninakupenda!” Yesu akamwambia tena: “Chunga kondoo wangu.”
Nao waliposikia maneno hayo, wakamusifu Mungu. Na kisha wakamwambia Paulo: “Ndugu, unaona namna maelfu ya Wayuda walivyoamini; nao wote wanajitolea sana kwa kushika Sheria.