Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 15:28 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

28 Ndugu huyu mukubwa akakasirika na kukataa kuingia ndani ya nyumba. Basi baba yake akatoka inje na kumusihi aingie.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 15:28
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wanawaambia wale wanaokutana nao hivi: Muikae mbali nami; musinikaribie kwa sababu mimi ni mutakatifu! Watu hao wananikasirikisha sana, hasira yangu ni kama moto usiozimika.


Musikilize neno la Yawe, enyi munaotetemeka kwa sababu ya neno lake. Wandugu zenu ambao wanawachukia, na kuwafukuza kwa sababu yangu, wamesema hivi kwa kuwachekelea: Mungu aonyeshe utukufu wake, nasi tuwaone ninyi mukishinda! Lakini wao wenyewe ndio watakaopata haya!


Wana wa Yonadabu mwana wa Rekabu wameshika amri waliyopewa na babu yao; lakini ninyi hamukunitii.


Lakini Mungu akamwuliza Yona: Unazani unafanya vema kuukasirikia mumea huo? Yona akajibu: Ndiyo, ninafanya vema kukasirika – kukasirika hata kufa!


Watu wale walipopokea mushahara ule, wakamunungunikia mwenye shamba.


Mutu mumoja mwenye ukoma alikuja kwa Yesu, akapiga magoti mbele yake na kumusihi, akisema: “Kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema, wewe unayewaua manabii na wajumbe ambao Mungu anakutumia kwa kuwatupia mawe. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Wafarisayo na walimu wa Sheria wakaanza kunungunika, wakisema: “Mutu huyu anawakaribisha watenda mabaya na kula pamoja nao!”


Mutumishi ule akamujibu: ‘Mudogo wako amerudia salama; kwa hiyo baba yako amechinja yule ngombe mwenye kunona.’


Lakini akamujibu baba yake: ‘Ninakutumikia kwa miaka mingi na sijakukosea hata mara moja. Ingawa vile haujanipatia hata kitoto cha mbuzi kusudi nifurahi pamoja na warafiki zangu.


Iliandikwa vilevile kwamba kwa jina lake watahubiri mataifa yote, kuanzia Yerusalema, kusudi wageuke toka katika zambi na wapate kusamehewa.


Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”


Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”


Wayuda walipoona lile kundi la watu, wakajaa na wivu sana, nao wakapinga maneno Paulo aliyosema na kumutukana.


Lakini Wayuda wakawashawishi wakubwa wa muji pamoja na wanawake wamoja wenye heshima, walioabudu Mungu. Wakawatesa Paulo na Barnaba hata wakawafukuza toka katika inchi yao.


Kisha Wayuda wamoja wakakuja tokea katika muji wa Antiokia na wa Ikonio. Wakashawishi makundi ya watu wajiunge nao. Wakamutupia Paulo mawe na kumukokotea inje ya muji, wakizani kwamba amekwisha kufa.


Lakini Wayuda waliokataa kuamini walishawishi watu wa mataifa mengine na kuwasukuma kuwachukia wandugu waamini.


Ninauliza tena: Waisraeli hawakufahamu kitu? Kwanza Musa alikuwa amekwisha kujibu: “Nitawafanya kuwa na wivu juu ya watu wasiokuwa taifa. Nitawakasirikisha ninyi kwa njia ya taifa pumbafu.”


Basi sisi ni wajumbe wa Kristo. Kwa njia yetu, Mungu mwenyewe anawaita ninyi; na kwa hiyo tunawasihi katika jina la Kristo, mukubali kupatanishwa na Mungu.


Wanajikaza kutuzuiza tusitangaze Habari Njema kwa watu wa mataifa mengine kusudi wasiokoke. Hivi wanafikilia kwenye hatua ya mwisho ya zambi walizotenda siku zote. Lakini kwa mwisho kasirani ya Mungu imewaangukia.


Lakini Eliabu, kaka mukubwa wa Daudi alipomusikia Daudi akiongea na watu, alimukasirikia Daudi, akasema: “Kwa nini umekuja? Wale kondoo wachache umemwachia nani kule katika mbuga? Ninajua majivuno yako na uovu wa moyo wako. Umekuja tu kutazama vita.”


Saulo hakupendezwa na maneno ya wimbo huo. Akakasirika sana. Akasema: “Wamemupa Daudi elfu makumi, lakini mimi wamenipa maelfu tu. Linalobakia ni kumupa Daudi ufalme.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ