Mwana wa Mutu alikuja, yeye anakula na kunywa, nao wanasema: ‘Angalia huyu mulafi na mulevi, rafiki wa walipishaji wa kodi na watenda maovu wenzao.’ Lakini hekima ya Mungu ilionyeshwa kuwa ya haki kwa njia ya matendo yake.”
Nao Wafarisayo walipoona mambo hayo, wakawaambia wanafunzi wake: “Kwa sababu gani mwalimu wenu anakula pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”
Wafarisayo na walimu wa Sheria wa kikundi chao wakawanungunikia wanafunzi wake, wakisema: “Kwa sababu gani munakula na kunywa pamoja na walipishaji wa kodi na watenda mabaya?”
Yule Mufarisayo aliyemwalika Yesu alipoona vile, akajisemesha: “Kama mutu huyu angekuwa kweli nabii, angetambua mwanamuke huyu anayemugusa ni wa namna gani. Angetambua kwamba yeye ni mwenye mwenendo mubaya.”
Kwa maana mbele ya kufika kwa watu wamoja waliotumwa na Yakobo kule, yeye alizoea kula pamoja na watu wa mataifa mengine. Lakini watu wale walipofika, akajitenga na kuacha kula pamoja na watu wa mataifa mengine, kwa sababu ya kuogopa wale wanaolazimisha kutahiriwa.
Neno hili ni la kuaminiwa nalo linastahili kukubaliwa kabisa: Kristo Yesu alikuja katika dunia kwa kuokoa wenye zambi. Na mimi ni wa kwanza mwenye zambi kati yao,