Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.
Unapokuwa sasa mabomoko matupu, Yerusalema unakumbuka utukufu wake. Ulipoangukia katika mikono ya waadui zake, hakuna aliyekuwa pale kwa kuusaidia. Washindi wake walichekelea kuanguka kwake.
Mama yao amefanya uzinzi, aliyebeba mimba yao amefanya mambo ya haya. Alisema: Nitaambatana na wapenzi wangu, ambao wananipatia chakula na maji, nguo za sufu na kitani, pamoja na mafuta na divai.
Watu wakakuja kusudi waone jambo lile. Walipofika kwa Yesu, wakamukuta yule mutu aliyetokwa na pepo akiikaa mbele ya Yesu, akiwa amevaa nguo, nayo akili yake ikiwa sawa. Basi watu wale wakaogopa.
Petro alipotambua kwamba mambo yaliyotokea ni ya kweli akasema: “Sasa ninajua hakika kwamba Bwana alimutuma malaika wake kuniokoa katika mikono ya Herode na katika mabaya yote Wayuda waliotaka kunitendea.”
Kwa maana yote yanayoonekana wazi yanageuka mwangaza. Ni kwa hiyo inasemwa hivi: “Amuka wewe unayelala! Ufufuke kutoka kati ya wafu, naye Kristo atakuangazia.”