Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 15:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Kwa hiyo akaenda kuomba kazi kwa mukaaji mumoja wa inchi ile. Mukaaji yule akamutuma katika mashamba yake kufanya kazi ya kukulisha nguruwe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 15:15
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati alipokuwa katika taabu zaidi, mufalme huyu Ahazi alizidi kumwasi Yawe.


Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.


Niwapige wapi tena, ninyi munaoendelea kuasi? Kichwa chote kinajaa vidonda, na moyo unaumia kabisa!


Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao; niliwaazibu, nikauficha uso wangu na kukasirika. Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


Wewe utaibeba haya yako kabisa! Zambi zako ni mbaya zaidi kuliko za wadada zako, kwa kipimo cha kuwafanya wadada zako na zambi zao, waonekane kama hawana kosa. Basi, upate haya na kufezeheka, maana umewafanya wadada zako waonekane kama hawana kosa.


Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.


Nitakutupia uchafu, na kukuzaraulisha, na kukufanya kuwa mushangao kwa watu.


Nami vilevile nitawafanya muzarauliwe na kuchekelewa na Waisraeli, kwa sababu hamukuzifuata njia zangu, na munapowafundisha watu wangu munapendelea wamoja kati yao. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.


“Musiwape imbwa vitu vitakatifu, kusudi wasiwageukie na kuwararua, wala musiwatupie nguruwe ushanga zenu za bei kusudi wasizikanyagekanyage.


Nyuma ya siku chache, yule mudogo akauzisha urizi wake na kwenda katika inchi ya mbali. Kule aliponda mali yake yote katika maisha ya ovyo.


Alipokwisha kumaliza mali yake yote, njaa kubwa ikatokea katika inchi ile, akaanza kuishi katika ukosefu.


Naye alitamani sana kula maganda yale nguruwe waliyokula, lakini hakuna mutu aliyemupa nayo.


Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.


Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ