Basi, Musa na Haruni wakamwendea mufalme wa Misri na kumwambia: “Yawe, Mungu wa Waebrania, anasema hivi: ‘Mpaka wakati gani utakataa kujinyenyekeza mbele yangu? Uwaache watu wangu waondoke kusudi wanitumikie.
Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.
Wewe utaibeba haya yako kabisa! Zambi zako ni mbaya zaidi kuliko za wadada zako, kwa kipimo cha kuwafanya wadada zako na zambi zao, waonekane kama hawana kosa. Basi, upate haya na kufezeheka, maana umewafanya wadada zako waonekane kama hawana kosa.
Nitakusamehe kila kitu ulichotenda. Nawe utakapokumbuka hayo yote uliyotenda utashangaa na kunyamaza kwa sababu ya haya wala hautasubutu kusema tena. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.
Nami vilevile nitawafanya muzarauliwe na kuchekelewa na Waisraeli, kwa sababu hamukuzifuata njia zangu, na munapowafundisha watu wangu munapendelea wamoja kati yao. –Ni Yawe wa majeshi anayesema hivyo.
Lakini sasa kufuatana na vile mumewekwa huru toka utawala wa zambi na kugeuka watumwa wa Mungu, munapata faida ya kuishi katika utakatifu na kwa mwisho kupewa uzima wa milele.
Kwa maana zamani sisi vilevile tulikuwa wajinga, waasi na wapotovu. Tulikuwa tumetawaliwa na kila namna ya tamaa mbaya na ya vitu mbalimbali vilivyotuvuta sana. Tuliishi katika uovu na wivu, tuliwachukiza watu nao walituchukia.