Kisha akasema: Ee Bwana wangu, kama nimepata kukubaliwa mbele yako, ninakuomba uende pamoja nasi. Watu hawa ni wenye vichwa vigumu, lakini utusamehe uovu wetu na zambi yetu, utupokee kama watu wako mwenyewe.
Kisha Yawe akaniambia: Hata kama Musa na Samweli wangesimama mbele yangu na kunisihi, singewahurumia watu hawa. Uwaondoe kabisa mbele yangu. Uwaache waende!
Mutu analipwa mabaya kwa mema? Lakini, wamenichimbia shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele yako, nikasema mema kwa ajili yao, kusudi niepushe hasira yako mbali nao.
Kati ya mazabahu na mulango wa hekalu, makuhani wanaomutumikia Yawe, walie na kuomba wakisema: Uwahurumie watu wako, ee Yawe. Usiyaache mataifa mengine yatuzarau na kutuchekelea yakisema: Yuko wapi basi Mungu wao?
Basi akamwambia mutunzaji wa hili shamba: ‘Sasa ni muda wa miaka mitatu ninakuja kutafuta matunda juu ya muti huu wa tini nami sipati kitu. Uukate! Muti huu unaharibu udongo bure.’
Bwana hakawii kutimiza ahadi zake kama vile watu wamoja wanavyozania. Yeye anavumilia kwa ajili yenu, maana hapendi hata mutu mumoja apotee, lakini anataka watu wote wageuke toka zambi zao.