Luka 13:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Kisha Yesu akawaambia mufano huu: “Mutu mumoja alikuwa na muti wa tini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu. Alikuja kutafuta matunda juu yake, lakini hakupata kitu.
Lakini mimi nilikupanda kama mizabibu uliochaguliwa, muzabibu wenye afya na wa mbegu safi. Mbona basi umeharibika, umegeuka kuwa muzabibu wa bure wa pori?
Nilitaka kuchuma matunda kutoka kwao. –Ni ujumbe wa Yawe.– Lakini sikupata zabibu hata moja juu ya muzabibu, sikupata tini zozote juu ya muti wa tini; hata majani yao yamekauka. Hata nilichokuwa nimewapa kimetoweka.
Ninyi hamukunichagua mimi, lakini ni mimi niliyewachagua ninyi. Nami nimewatuma muende kuzaa matunda yasiyokuwa na mwisho. Kwa hiyo Baba atawapa chochote munachoomba kwa jina langu.