Kwa hiyo, nitawahukumu ninyi Waisraeli, kila mumoja wenu, kulingana na mwenendo wake. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Mugeuke na kuachana na makosa yenu yasipate kuwaangamiza.
Vilevile munazani kwamba wale watu kumi na wanane waliokufa munara ulipowaangukia kule Siloamu, walikuwa wakosaji kuliko wakaaji wengine wote wa Yerusalema?
Kisha Yesu akawaambia mufano huu: “Mutu mumoja alikuwa na muti wa tini uliopandwa katika shamba lake la mizabibu. Alikuja kutafuta matunda juu yake, lakini hakupata kitu.