Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 13:34 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

34 “Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema, wewe unayewaua manabii na wajumbe ambao Mungu anakutumia kwa kuwatupia mawe. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 13:34
46 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini hawakukuwa waaminifu kwako. Wakakuasi, wakaacha sheria yako na kuwaua manabii waliowaonya kusudi wakurudilie wewe. Wakatenda zambi kubwa mbele yako.


Ukawavumilia kwa miaka mingi, na kuwaonya kwa njia ya roho wako kwa kupitia manabii wako; hata hivyo hawakusikiliza. Basi ukawaacha ukawatia katika mikono ya mataifa mengine.


Umufurahie Muumba wako, ee Israeli; ninyi wakaaji wa Sayuni, mumushangilie mufalme wenu.


Unilinde kama mboni ya jicho lako; unifiche chini ya kivuli cha mabawa yako,


Haki yako ni kama milima mikubwa, hukumu zako ni kama vilindi vya bahari. Wewe, ee Yawe, unawalinda wanadamu na nyama.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu.” Mashairi ya Daudi alipomuponyoka Saulo na kujificha katika pango.


Hivyo, nikawaacha wabaki katika ugumu; wafuate mashauri yao wenyewe.


Atakufunika kwa mabawa yake; utapata usalama kwake. Uaminifu wake ni ngao ya kukinga.


Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa; kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu. Lakini ninyi hamukutaka.


Nilipokuja, kwa nini sikukuta mutu? Nilipoita mbona hamukuitikia? Mukono wangu ni mufupi hata nisiweze kuwaokoa ninyi? Sina nguvu ya kuwakomboa? Ninakausha bahari kwa kuikaripia, na mito ninaifanya kuwa jangwa; samaki wake wanakufa na kunuka kwa kukosa maji.


Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.


Wao wakamurudisha Uria kutoka Misri, wakamupeleka kwa mufalme Yoyakimu. Mufalme akamwua kwa upanga na maiti yake ikatupwa katika kaburi.


Ile amri ambayo Yonadabu mwana wa Rekabu aliwapa wana wake kwamba wasikunywe divai, imefuatwa; nao hawakunywi divai mpaka siku hii ya leo, maana wametii amri ya babu yao. Lakini mimi nilisema nanyi tena na tena, nanyi hamukunisikiliza.


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli anasema hivi: Ninawaletea Wayuda na wakaaji wote wa Yerusalema hasara zote nilizosema juu yao, kwa sababu mimi nilisema nao, lakini hawakunisikiliza; niliwaita, lakini hawakuniitikia.


Yawe anasema hivi: Musimame katika masanganjia, muangalie. Muulize juu ya matukio ya zamani. Mutafute pahali panapokuwa njia nzuri muifuate, nanyi mutaweza kupumzika. Lakini wao wakasema: Hatutafuata njia hiyo.


Kwa sababu ya hayo ninalia, machozi yananitiririka, sina mutu yeyote wa kunifariji; hakuna yeyote wa kunitia moyo. Watoto wangu wameachwa ukiwa, maana adui yangu amenishinda.


Ni kwa sababu ya zambi za manabii wake na makosa ya makuhani wake, ambao walimwanga damu ya watu wa haki katika muji wake.


Lakini kadiri nilivyozidi kuwaita, ndivyo walivyozidi kwenda mbali nami; waliendelea kuyatambikia Mabali, na kuvifukizia ubani sanamu za miungu.


Watu wangu wamekusudia kuniacha mimi, wakiitwa kusimama wapande juu, hakuna hata mumoja anayeweza.


Mufurahi, enyi watu wa Sayuni, mushangilie kwa sababu ya Yawe, Mungu wenu, maana amewapa mvua zinazowafalia, amewapa mvua ya kutosha: mvua za kwanza na mvua za katikati kama pale mbele.


Musikuwe kama babu zenu. Manabii waliwaambia: Yawe anasema hivi: muachane na mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya. Lakini wao hawakunisikiliza wala hawakunitii. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Yeye akawatuma watumishi wake kwa kuwaita watu wale walioalikwa kwa karamu, lakini hawakutaka kufika.


na wengine wakawakamata wale watumishi wakawatesa na kuwaua.


Ndugu huyu mukubwa akakasirika na kukataa kuingia ndani ya nyumba. Basi baba yake akatoka inje na kumusihi aingie.


Watakuharibu kabisa pamoja na wakaaji wako. Hawatakuachia hata jengo moja lisilobomolewa kwa sababu haukutambua wakati Mungu alipokuja kukuokoa.”


Yesu akawageukia na kuwaambia: “Ninyi wanawake wa Yerusalema, musinililie mimi, lakini mujililie ninyi wenyewe pamoja na watoto wenu.


Ni nani kati ya manabii ambaye babu zenu walikosa kumutesa? Waliwaua wale waliotabiri zamani habari za kuja kwa Mwenye Haki. Na sasa mumemutoa na kumwua.


Walipokuwa wakimutupia mawe, Stefano akaomba akisema: “Ee Bwana Yesu, pokea roho yangu.”


Naye Saulo alikuwa amekubali kwamba Stefano anastahili kuuawa. Siku ile ile kanisa lililokuwa katika Yerusalema lilianza kupata mateso makubwa. Waamini wote walisambaa katika Yudea na Samaria, isipokuwa mitume tu.


Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa, wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwa namna gani.


Heri wangekuwa siku zote na mawazo kama haya wakiniheshimu na kushika amri zangu! Mambo yao yote yangewaendekea vizuri, wao wenyewe na wazao wao milele.


Maiti zao zitabaki katika barabara ya muji ule mukubwa unaoitwa kwa fumbo Sodoma au Misri. Ni ndani ya muji ule Bwana wao alitundikwa juu ya musalaba.


Yawe akubariki kwa yote uliyoyafanya. Yawe wa Israeli uliyemukimbilia akulinde chini ya mabawa yake, akupe zawadi kamilifu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ