Kwa sababu hii Yesu hakutembea tena akijionyesha waziwazi kati ya Wayuda. Kisha akajiendea pamoja na wanafunzi wake katika inchi iliyokuwa karibu na jangwa katika muji unaoitwa Efuraimu. Nao wakabaki kule.
Yesu akawaambia: “Mwangaza ungali kati yenu kwa muda kidogo. Mutembee wakati mungali na mwangaza, kusudi giza lisiwafunike, kwa sababu anayetembea katika giza hajui pahali anapokwenda.
Tena ninyi munajua namna Mungu alivyomuchagua Yesu wa Nazareti kwa kazi yake, akimujaza na Roho Mutakatifu na kumupatia uwezo. Naye alipita fasi zote akitenda mema na kuwaponyesha watu wote waliokuwa chini ya mamlaka ya Shetani. Ilitendeka vile kwa maana Mungu alikuwa pamoja naye.
Wakaaji wa Yerusalema na wakubwa wao hawakumutambua Yesu wala maandiko ya manabii yaliyosomwa kila siku ya Sabato. Lakini ingawa hivi wakatimiza maandiko yale kwa njia ya kumuhukumu kufa.