“Kisha mufalme atawaambia wale wanaokuwa kwa upande wake wa kushoto: ‘Muondoke hapa karibu nami, ninyi muliolaaniwa! Muende katika moto usiozimika hata milele, uliotayarishwa kwa ajili ya Shetani na wamalaika wake!
Na zaidi ya hii kuna shimo kubwa sana kati yetu na ninyi. Hivi wale wanaokuwa huku wakitaka kufika kule kwenu hawawezi, wala wale wanaokuwa kule hawawezi kuvuka kwa kufika huku kwetu.’
Wandugu, tunapaswa kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili yenu. Inatufaa kufanya vile kwa maana imani yenu inaongezeka, nao upendo wenu ninyi kwa ninyi unazidi kuongezeka.