Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Luka 12:48 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

48 Lakini kwa ngambo ingine, yule asiyejua mapenzi ya bwana yake, na anayefanya mambo yanayostahili azabu, atapigwa fimbo chache. Kwa maana kila mutu aliyepewa vingi, ataombwa kutoa vingi zaidi; na aliyepewa madaraka mengi, ataulizwa mengi zaidi.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Luka 12:48
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mutu yeyote akitenda zambi bila kujua, kwa kuvunja amri yoyote ya Yawe, yeye ana kosa, na atalipa azabu ya kosa lake.


Mutu mumoja akifanya zambi bila kujua, atatoa mbuzi dike wa mwaka mumoja kuwa sadaka kwa ajili ya zambi.


Kwa maana mutu anayekuwa na kitu ataongezewa kingine, naye atakuwa na vitu vingi. Lakini mutu asiyekuwa na kitu, ataondolewa hata kile kidogo anachokuwa nacho.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munanyanganya mali za wajane na kuomba maombi marefu kwa kujionyesha. Kwa sababu hii azabu yenu itakuwa kubwa zaidi!]


Halafu Petro akamwuliza Yesu: “Bwana, mufano huu unatuelekea sisi wenyewe au unawaelekea watu wote?”


“Nimekuja kuleta moto katika dunia, nami ningetaka sana kuona ukiwa umekwisha kuwaka!


Halafu bwana wake akamwita na kumwambia: ‘Ni habari gani ile waliyonielezea juu yako? Ninakuomba unifanyie hesabu yote ya mali yangu, kwa sababu hauwezi tena kuwa mulinzi wa mali yangu.’


Kama singekuja kusema nao, wasingekuwa na zambi; lakini sasa hawataweza kukana zambi yao.


Mungu hahesabu tena nyakati zile watu walipokuwa katika ujinga, lakini sasa anatangaza kwa watu wote, na nafasi zote kwamba wageuke toka zambi zao.


kama yule aliyehukumiwa amepewa azabu ya kupigwa fimbo, mwamuzi atamwamuru huyo alale chini na kupigwa fimbo kulingana na kosa lake.


Mafundisho haya yanalingana na Habari Njema ya utukufu wa Mungu mwenye baraka, ambayo nilipewa nipate kuihuburi.


Ingawa zamani nilikuwa mwenye kumutukana, mwenye kumutesa na kumutendea kwa ukali, lakini amenihurumia, kwa sababu yote niliyofanya, niliyafanya kwa upumbafu kwa maana sikukuwa bado na imani.


Timoteo, uchunge vizuri kile ulichopewa kwa kulinda, ukiepuka maneno ya kidunia na mabishano yasiyokuwa na maana juu ya ile watu wengine wanayoita kuwa ni elimu lakini ni uongo.


Alifunua neno lake kwa wakati alioupanga kwa njia ya mahubiri ambayo yeye Mungu Mwokozi wetu aliyoniamuru kutangaza.


Wandugu zangu, kati yenu kusikuwe walimu wengi, kwa maana munajua vema ya kuwa sisi walimu tutahukumiwa vikali zaidi kuliko watu wengine.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ