40 Kwa hiyo ninyi vilevile mukuwe tayari, kwa sababu Mwana wa Mutu atarudia saa musiyozania.”
Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku Bwana wenu atakaporudi.
Kwa hiyo, ninyi vilevile mukuwe tayari, kwa sababu Mwana wa Mutu atarudi saa musiyozania.
Na Yesu akaongeza kusema: “Basi mukeshe, kwa sababu hamujui siku wala saa ile.
Mufanye vile, maana munajua tunaishi katika siku gani sasa. Saa ya kuamuka katika usingizi wenu imetimia, kwa maana sasa wakati wetu wa kuokolewa unakaribia kuliko vile ilivyokuwa wakati tulipoanza kuamini.
Lakini Bwana Yesu akuwe kama vile silaha munayobeba, musijiachilie kuvutwa na hali yenu ya kimwili hata mutimize tamaa zake.
Basi tusilale usingizi kama vile wengine, lakini tukeshe na kuwa wakadirifu.
Tufurahi na kushangilia na kumutukuza, kwa sababu saa ya ndoa ya Mwana-Kondoo imetimia, naye bibi arusi wake amejitayarisha.”